-
Imani Katika Unabii wa Biblia Inaokoa UhaiMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
-
-
Katika muda wa miezi mitatu, gavana Mroma wa Siria, Sesho Galo, anashuka kusini akiwa na askari-jeshi 30,000 ili kuzima uasi wa Wayahudi. Jeshi lake linafika Yerusalemu wakati wa Sherehe ya Vibanda na kuingia moja kwa moja vijijini. Wayahudi waasi ambao ni wachache wanakimbilia katika ngome ya hekalu. Muda si muda, askari-jeshi Waroma wanaanza kuuharibu ukuta wa hekalu. Wayahudi wanaudhika, kwa sababu, askari-jeshi wapagani sasa wanatia unajisi mahali patakatifu zaidi pa dini ya Kiyahudi! Hata hivyo, Wakristo walio jijini wanakumbuka maneno haya ya Yesu: ‘Mtakapoona lile chukizo, likiwa limesimama katika mahali patakatifu, wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani.’ (Mathayo 24:15, 16) Je, wangeonyesha imani katika maneno ya Yesu ya kinabii na hivyo kuchukua hatua inayofaa? Kama ilivyotukia, uhai wao ulitegemea kufanya hivyo. Lakini wangekimbia jinsi gani?
Kwa ghafula na bila sababu yoyote nzuri, Sesho Galo anawaondoa askari-jeshi wake na kuelekea pwani huku wakikimbizwa mbio na Wayahudi waasi. Kwa kushangaza, dhiki juu ya jiji hilo ilikuwa imefupishwa! Wakristo wanaonyesha imani yao katika onyo la kinabii la Yesu na kutoka Yerusalemu na kukimbilia Pela, jiji lisilomilikiwa na yeyote lililo milimani ng’ambo ya Mto Yordani. Wanakimbia kwa wakati unaofaa kabisa. Punde si punde, Wayahudi hao waasi wanarudi Yerusalemu na kuwalazimisha watu waliobaki jijini kuunga mkono uasi wao.a Wakristo wakiwa salama huko Pela, wanangojea matukio mengine.
-
-
Imani Katika Unabii wa Biblia Inaokoa UhaiMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
-
-
a Mwanahistoria Myahudi Yosefo anaripoti kwamba Wayahudi waasi waliwafuata Waroma kwa siku saba kabla ya kurudi Yerusalemu.
-