Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Njia Ambayo Watumishi wa Yehova Hufundishwa

      Yesu Kristo alitabiri kwamba baada ya kurudi kwake mbinguni, yeye angepelekea wanafunzi wake roho takatifu. Hiyo ingetumikia ikiwa msaidizi, ikiwaongoza “ndani ya kweli yote.” (Yn. 14:26; 16:7, 13, NW) Pia Yesu alisema kwamba akiwa Bwana au Bwana-Mkubwa wa Wakristo wa kweli, yeye angekuwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” au “msimamizi-nyumba mwaminifu,” ambaye angetoa ‘chakula cha kiroho kwa wakati ufaao’ kwa watu wa nyumbani, wale wafanyakazi katika watu wa nyumba ya imani. (Mt. 24:45-47; Luka 12:42, NW) Huyo mtumwa mwaminifu na mwenye busara ni nani?

      Toleo lilelile la kwanza la Watch Tower liligusia Mathayo 24:45-47 lilipotaarifu kwamba lengo la watangazaji wa gazeti hilo lilikuwa kuwaweka chonjo kuona matukio yenye kuhusiana na kuwapo kwa Kristo na kuwapa “nyama [ya kiroho] kwa majira yake” watu wa nyumba ya imani. Lakini mhariri wa gazeti hilo hakuwa mwenyewe akidai kuwa ndiye huyo mtumwa mwaminifu mwenye busara, au “mtumishi mwaminifu na mwenye hekima” (kulingana na tafsiri ya King James Version).

      Hivyo, katika toleo la Oktoba-Novemba 1881 la gazeti hilo, C. T. Russell alitaarifu hivi: “Sisi twaamini kwamba kila mshiriki wa mwili huo wa Kristo anashiriki katika kazi hii iliyobarikiwa, ama moja kwa moja ama kwa njia isiyo ya moja kwa moja, ya kuwapa nyama kwa majira yake watu wa nyumba ya imani. ‘Ni nani basi huyo mtumwa mwaminifu mwenye hekima ambaye Bwana wake amemfanya mtawala juu ya watu wa nyumba yake,’ awape nyama kwa majira yake? Je, si hilo ‘kundi dogo’ la watumishi waliojitakasa ambao wanatimiza kwa uaminifu nadhiri zao za kujitakasa—ule mwili wa Kristo—na je, mwili wote ukiwa watu mmoja-mmoja na wote kwa ujumla, hauwapi nyama kwa majira yake watu wa nyumba ya imani—ule ushirika mkubwa wa waamini? Mbarikiwa ni mtumishi huyo (ule mwili mzima wa Kristo) ambaye Bwana wake ajapo (Kigiriki elthon) atamkuta akifanya hivyo. ‘Kweli, nawaambia, kwamba atamfanya kuwa mtawala juu ya mali yake yote.’”

  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Uelewevu uliotolewa na Ndugu Russell katika 1881 kwamba mtumishi mwaminifu mwenye hekima alikuwa kwa kweli mtumishi wa ujumla, akitia ndani washiriki wote wa mwili wa Kristo waliotiwa mafuta kwa roho walioko duniani, ulithibitishwa tena katika The Watch Tower la Februari 15, 1927.—Linganisha Isaya 43:10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki