-
‘Yule Mtumwa Mwaminifu’ Apita Mtihani wa Ukaguzi!Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 1
-
-
Akampa mmoja talanta tano, mwingine mbili, na mwingine moja, kila mmoja kulingana na uwezo wake mwenyewe, naye akaenda ng’ambo.” (Mathayo 25:14, 15)
-
-
‘Yule Mtumwa Mwaminifu’ Apita Mtihani wa Ukaguzi!Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 1
-
-
Kwa maneno hayo Yesu aliwapa “watumwa” wake ruhusa ya kufanya biashara hadi atakaporudi, “kila mmoja kulingana na uwezo wake mwenyewe.”
14. Kwa nini wanafunzi wote hawakutazamiwa wafanye biashara kwa kiwango kilekile?
14 Maneno hayo yanaonyesha kwamba hali za Wakristo wote wa karne ya kwanza hazikufanana. Hali za wengine, kama vile Paulo na Timotheo, ziliwawezesha kushiriki kikamili katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. Huenda hali za wengine zilifanya iwe vigumu sana kushiriki katika kazi hiyo. Kwa mfano, Wakristo fulani walikuwa watumwa, wengine walikuwa wagonjwa, wazee, au wenye madaraka ya familia. Bila shaka, kulikuwa na mapendeleo fulani kutanikoni ambayo baadhi ya wanafunzi hawakuyapata. Baadhi ya wanawake na wanaume watiwa-mafuta hawakufundisha kutanikoni. (1 Wakorintho 14:34; 1 Timotheo 3:1; Yakobo 3:1) Hata hivyo, bila kujali hali zao, wanafunzi wote wa Kristo waliotiwa mafuta, wanaume kwa wanawake, walipewa mgawo wa kufanya biashara, nao walitumia vizuri nafasi na hali zao katika huduma ya Kikristo. Leo wanafunzi wa Kristo hufanya vivyo hivyo.
-