-
Jambo la Kufanya Unapoudhi WengineAmkeni!—1996 | Februari 8
-
-
iache sadaka [“zawadi,” NW] yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka [“zawadi,” NW] yako.”
-
-
Jambo la Kufanya Unapoudhi WengineAmkeni!—1996 | Februari 8
-
-
‘Iache Zawadi Yako Uende Zako’
“Iache sadaka [“zawadi,” NW] yako mbele ya madhabahu,” Yesu aeleza, “uende zako.” Kwa nini? Ni nini kingekuwa cha maana zaidi wakati huo kuliko kumtolea Yehova dhabihu? “Kwanza fanya amani yako na ndugu yako,” (NW) Yesu aendelea kueleza, “kisha urudi uitoe sadaka [“zawadi,” NW] yako.” Kwa hiyo huyo mwabudu aacha toleo lake likiwa hai kwenye madhabahu ya toleo la kuteketezwa naye aenda zake kumtafuta ndugu yake aliyeudhika.
Kwa kuwa ni sikukuu, ndugu yake aliyeudhika bila shaka yumo miongoni mwa wasafiri ambao wamemiminikia Yerusalemu. Kukiwa na barabara nyembamba na nyumba ambazo zimesongamana pamoja, Yerusalemu lina wakazi wengi. Lakini hii ni sikukuu, na jiji limejaa wageni.b
Hata ikiwa watu kutoka mji mmoja walisafiri na kupiga kambi pamoja, kupitia hilo jiji lililosongamana watu ili kumtafuta mtu fulani kungehitaji jitihada fulani. Kwa kielelezo, wakati wa Sikukuu ya Vibanda, wageni walijenga vibanda kotekote jijini na barabarani na bustanini kuzingira Yerusalemu. (Mambo ya Walawi 23:34, 42, 43) Hata hivyo, mwabudu Myahudi anapaswa amtafute ndugu yake aliyeudhika mpaka ampate. Kisha nini?
“Fanya amani yako na ndugu yako,” (NW) asema Yesu. Usemi uliofasiriwa “fanya amani yako” hutokana na kitenzi (di·al·lasʹso) kinachomaanisha “‘kuleta geuzo, kubadilishana,’ na kwa hiyo, ‘kupatanisha.’” Akiwa amejitahidi sana kumtafuta ndugu yake aliyeudhika, huyo mwabudu Myahudi anajaribu kufanya amani naye. Kisha, asema Yesu, yeye aweza kurudi hekaluni na kutoa zawadi yake, kwa maana sasa Mungu ataikubali.
Hivyo maneno ya Yesu kwenye Mathayo 5:23, 24 hufundisha somo muhimu: Upatanisho, au amani, huja kabla ya dhabihu. Njia ambayo sisi huwatendea waabudu wenzetu inahusiana moja kwa moja na uhusiano wetu na Mungu.—1 Yohana 4:20.
Jambo la Kufanya Unapoudhi Wengine
Namna gani basi, ukijipata mwenyewe katika hali iliyofafanuliwa mwanzoni mwa makala hii—unahisi kwamba umemuudhi mwabudu mwenzako? Wapaswa kufanya nini?
Ukitumia shauri la Yesu, chukua hatua ya kwanza ya kumwendea ndugu yako. Ukiwa na lengo jipi? Kumsadikisha kwamba yeye hana sababu ya kuudhika? La hasha! Huenda tatizo likawa kubwa zaidi ya kutoelewana kuliko sahili. “Fanya amani yako,” (NW) akasema Yesu. Ikiwezekana, ondoa uadui kutoka moyoni mwake. (Warumi 14:19) Ili kutimiza hilo, huenda ukahitaji kukiri, wala si kukanusha, hisia zake za kuudhika. Huenda ukahitaji pia kuuliza hivi, ‘Naweza kufanya nini ili kusahihisha mambo?’ Mara nyingi, kuomba radhi kwa moyo mweupe ndiko kunakohitajiwa tu. Hata hivyo, katika visa vingine mtu aliyeudhika huenda akahitaji wakati fulani ili kutuliza hisia zake.
Lakini, namna gani ikiwa zijapokuwa jitihada za mara kwa mara wewe huwezi kuleta upatanisho? Warumi 12:18 husema hivi: “Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.” Hivyo waweza kuwa na uhakika kwamba maadamu umejitahidi sana kufanya amani, Yehova atapendezwa kukubali ibada yako.
-