Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, “Hekima ya Kutoka Juu” Inakuongoza Maishani?
    Mkaribie Yehova
    • 11 Unapaswa kufanya nini ukigundua kwamba umemkosea mwabudu mwenzako? Yesu alisema: “Basi, ikiwa wewe unaleta zawadi yako kwenye madhabahu na huko wakumbuka kwamba ndugu yako ana jambo fulani dhidi yako, acha zawadi yako hapo mbele ya madhabahu, na uende zako; kwanza fanya amani yako na ndugu yako, na ndipo, ukiisha kurudi, toa zawadi yako.” (Mathayo 5:23, 24) Unaweza kutumia shauri hilo kwa kuchukua hatua ya kwenda kumwona ndugu yako. Ukiwa na kusudi gani? Ili ‘ufanye amani yako’ naye.b Ili kutimiza kusudi hilo, huenda ukahitaji kukubali kwamba umemwumiza kihisia. Ukimfikia kwa kusudi la kufanya amani na udumishe mtazamo huo, yaelekea kwamba tatizo litasuluhishwa, utaomba msamaha na utasamehewa. Unapochukua hatua ya kufanya amani, unaonyesha kwamba unaongozwa na hekima ya Mungu.

  • Je, “Hekima ya Kutoka Juu” Inakuongoza Maishani?
    Mkaribie Yehova
    • b Usemi wa Kigiriki unaotafsiriwa “fanya amani yako” unatokana na kitenzi kinachomaanisha “‘kuleta badiliko, kubadilishana,’ na hivyo, ‘kupatanisha.’” Kwa hiyo, kusudi lako ni kubadilisha hali, na ikiwezekana, kuondoa chuki iliyo moyoni mwa yule aliyekosewa.—Waroma 12:18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki