-
Kuazimia Kuwa Tajiri KirohoAmkeni!—2007 | Juni
-
-
Kuazimia Kuwa Tajiri Kiroho
ILI mtu awe tajiri kimwili anahitaji kuendelea kujitahidi na kujinyima mambo fulani. Ndivyo ilivyo na kuwa tajiri kiroho. Yesu alidokeza jambo hilo aliposema hivi: “Jiwekeeni hazina mbinguni.” (Mathayo 6:20) Hazina za kiroho hazitokei zenyewe tu. Mtu hawezi kuwa tajiri kimwili kwa sababu tu ana akaunti ya benki. Vivyo hivyo, hawezi kuwa tajiri kiroho eti kwa sababu tu ana dini. Ili mtu asitawishe uhusiano wa karibu pamoja na Mungu, awe mtu wa kiroho, na awe na sifa nyingi za kiroho anahitaji kuwa na azimio, wakati, kuendelea kujitahidi, na kujinyima mambo fulani.—Methali 2:1-6.
-
-
Kuazimia Kuwa Tajiri KirohoAmkeni!—2007 | Juni
-
-
Faida Zisizo na Kifani
Tofauti na hazina zilizo duniani, ambazo wezi wanaweza kuiba, utajiri wa kiroho ni wa kudumu. (Methali 23:4, 5; Mathayo 6:20) Ni kweli kwamba ni vigumu kupima maendeleo ya kiroho. Ni rahisi zaidi kupima maendeleo ya mtu ya kimwili kuliko ilivyo kupima maendeleo yake katika kukuza upendo, shangwe, au imani. Lakini faida za utajiri wa kiroho hazina kifani. Akizungumza kuhusu wanafunzi ambao wangeacha hata nyumba zao na mashamba yao, yaani, njia yao ya kupata riziki, ili kuwa na nafasi kwa ajili ya mambo ya kiroho, Yesu alisema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Hakuna mtu ambaye ameacha nyumba au ndugu au dada au mama au baba au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema ambaye hatapata mara mia sasa katika kipindi hiki cha wakati, nyumba na ndugu na dada na mama na watoto na mashamba, pamoja na mateso, na katika mfumo wa mambo unaokuja uzima wa milele.”—Marko 10:29, 30.
Utatanguliza nini? Mungu au mali?
-