-
Je, Kuhangaika Kunaonyesha Kwamba Mtu Hana Imani?Amkeni!—2004 | Juni 8
-
-
Maoni ya Biblia
Je, Kuhangaika Kunaonyesha Kwamba Mtu Hana Imani?
“MAHANGAIKO YAMEPIGWA MARUFUKU.” Mwanzoni mwa karne ya 20, padri mmoja aliandika makala yenye kichwa hicho. Katika makala hiyo aliandika kwamba kuhangaikia vitu vya kimwili si kosa tu bali ni “dhambi nzito sana.” Hivi karibuni, mtu mmoja aliandika hivi kuhusu kushinda wasiwasi na mahangaiko: “Tukiwa na wasiwasi, ni wazi kwamba hatumwamini Mungu.”
Waandishi hao wawili walifikia mkataa wao kwa kutumia Mahubiri ya Mlimani ya Yesu, ambapo alisema: “Acheni kuhangaika.” (Mathayo 6:25) Kwa kuwa watu wengi sana leo huhangaika, tunaweza kuuliza hivi: Je, Mkristo anapaswa kuhisi hatia kwa kuhangaika? Je, kuhangaika kunaonyesha kwamba mtu hana imani?
-
-
Je, Kuhangaika Kunaonyesha Kwamba Mtu Hana Imani?Amkeni!—2004 | Juni 8
-
-
Mungu Anajua Mahitaji Yetu
Maandiko hutusaidia kutofautisha mahangaiko ya kawaida na ile dhambi ya ukosefu wa imani. Kuwa na mahangaiko ya kila siku au hata kukosa imani kidogo kwa sababu ya udhaifu wa kibinadamu si sawa na kukosa kumtumaini Mungu kabisa kunakotokana na moyo mwovu na mgumu. Kwa hiyo, Wakristo hawapaswi kuhisi hatia kwa sababu ya mahangaiko yao ya mara kwa mara.
Hata hivyo, tunapaswa kuwa waangalifu ili mahangaiko yetu yasipite kiasi na kutulemea. Ndiyo sababu Yesu alisema maneno haya ya hekima: “Msihangaike kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’” Kisha akaongeza maneno haya yenye kufariji: “Kwa maana Baba yenu wa mbinguni anajua mnahitaji vitu hivi vyote. Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake, nanyi mtaongezewa hivi vitu vingine vyote.”—Mathayo 6:25-33.
-