Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sitawisha Ile Roho ya Aliye Mdogo Zaidi
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Novemba 15
    • 1, 2. Yesu aliwapa mitume wake shauri gani, na kwa nini?

      ULIKUWA mwaka wa 32 W.K. Yesu alikuwa katika wilaya ya Galilaya wakati matatizo yalipotokea. Baadhi ya mitume wake walikuwa wakibishana kuhusu ni nani aliye mkuu zaidi kati yao. Luka, mwandikaji wa Injili, anaripoti hivi: “Wakaanza kujadiliana kati yao kuhusu ni nani angekuwa mkuu zaidi kati yao. Yesu, akijua mawazo ya mioyo yao, akachukua mtoto mchanga, akamweka kando yake na kuwaambia: ‘Yeyote yule anayempokea mtoto huyu mchanga kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia, na yeyote anayenipokea, anampokea pia yule aliyenituma. Kwa maana anayejiendesha kama aliye mdogo zaidi kati yenu nyote ndiye aliye mkuu.’” (Luka 9:46-48) Kwa subira, lakini kwa uthabiti, Yesu aliwasaidia mitume hao kutambua umuhimu wa kuwa wanyenyekevu.

      2 Je, shauri la Yesu la kujiendesha kama aliye mdogo zaidi lilipatana na mwelekeo wa Wayahudi wa karne ya kwanza? Au je, lilikuwa kinyume kabisa na mtazamo waliokuwa nao kwa ujumla? Kitabu kimoja (Theological Dictionary of the New Testament) kinasema hivi kuhusu mtazamo wa watu wengi wakati huo: “Katika kila jambo, swali kuhusu ni nani aliye mkuu zaidi ya wote lilizuka, na kumpa kila mtu heshima aliyostahili lilikuwa jambo muhimu lililowahangaisha watu kila mara.” Yesu alikuwa akiwashauri mitume wake wawe tofauti na watu kwa ujumla.

      3. (a) Kujiendesha kama aliye mdogo zaidi kunamaanisha nini, na kwa nini inaweza kuwa vigumu kwetu kujiendesha kwa njia hiyo? (b) Ni maswali gani yanayozuka kuhusu kusitawisha roho ya aliye mdogo zaidi?

      3 Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “aliye mdogo zaidi” linamaanisha mtu mwenye kiasi, mnyenyekevu, mpole, wa hali ya chini, na ambaye si mashuhuri. Yesu alitumia mtoto mchanga kuwaonyesha wazi mitume wake kwamba wanapaswa kuwa wanyenyekevu na wenye kiasi.

  • Sitawisha Ile Roho ya Aliye Mdogo Zaidi
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Novemba 15
    • Mtu anayejiendesha kama aliye mdogo zaidi ni “mkuu” katika maana ya kwamba anakuwa mtumishi mwenye thamani zaidi wa Yehova. (Luka 9:48) Acheni tuone inakuwaje hivyo.

      ‘ALIYE MDOGO ZAIDI KATI YENU NI MKUU’

      8. Unyenyekevu unatusaidia kuwa na mtazamo gani kuelekea tengenezo la Yehova?

      8 Ni muhimu sana tuwe wanyenyekevu ili turidhike katika tengenezo la kitheokrasi la Mungu na kuunga mkono mpango wa kutaniko. Kwa mfano, mfikirie Petra, mwanamke kijana aliyelelewa katika familia ya Mashahidi wa Yehova. Petra alijitenga na kutaniko kwa sababu alitaka kufanya mambo kwa njia yake mwenyewe. Baada ya miaka mingi kupita, alianza tena kushirikiana na kutaniko. Sasa, anafurahi kuwa katika tengenezo la Yehova na anaunga mkono kwa bidii mpango wa kutaniko. Ni nini kilichofanya abadili mtazamo wake? Anaandika hivi: “Ili nijihisi nikiwa sehemu ya tengenezo la Mungu, nilihitaji kuelewa na kusitawisha sifa mbili muhimu zaidi, unyenyekevu na kiasi.”

      9. Mtu mnyenyekevu ana mtazamo gani kuelekea chakula cha kiroho tunachopokea, na kwa nini jambo hilo linamfanya awe mwenye thamani zaidi?

      9 Mtu mnyenyekevu anathamini kutoka moyoni maandalizi ya Yehova, kutia ndani chakula cha kiroho. Kwa hiyo, mtu kama huyo hujifunza Biblia kwa bidii na anasoma kwa hamu magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kama tu watumishi wengine wengi waaminifu wa Yehova, anaweza kuwa na zoea la kusoma kila chapisho jipya kabla ya kuliweka kwenye maktaba yake. Tunapoonyesha unyenyekevu na uthamini kwa kusoma na kujifunza machapisho yetu yanayotegemea Biblia, tutafanya maendeleo ya kiroho, na Yehova ataweza kututumia kwa ukamili zaidi katika utumishi wake.​—Ebr. 5:13, 14.

      10. Tunaweza kuonyeshaje mtazamo wa aliye mdogo zaidi kutanikoni?

      10 Mtu anayejiendesha kama aliye mdogo zaidi ni “mkuu” katika njia nyingine. Kila kutaniko lina wanaume wenye sifa za kustahili waliowekwa rasmi chini ya mwongozo wa roho takatifu ya Yehova ili watumike wakiwa wazee. Wanapanga mambo ya kiroho kama vile mikutano ya kutaniko, utumishi wa shambani, na uchungaji. Tunapoonyesha mtazamo wa aliye mdogo zaidi kwa kuunga mkono kwa hiari mipango hiyo, tunachangia furaha, amani, na umoja kutanikoni. (Soma Waebrania 13:7, 17.) Ikiwa unatumika ukiwa mzee au mtumishi wa huduma, je, humshukuru Yehova kwa unyenyekevu kwa kukukabidhi pendeleo hilo la utumishi?

      11, 12. Ni mtazamo gani utakaotufanya tuwe wenye thamani zaidi katika tengenezo la Yehova, na kwa nini inakuwa hivyo?

      11 Mtu anayejiendesha kama aliye mdogo zaidi ni “mkuu,” au ana thamani zaidi katika tengenezo la Yehova kwa sababu unyenyekevu wake unamfanya awe mtumishi muhimu wa Mungu. Yesu alilazimika kuwashauri wanafunzi wake wajiendeshe kama walio wadogo zaidi kwa sababu baadhi yao waliathiriwa na roho iliyokuwa imeenea wakati huo. Andiko la Luka 9:46 linasema hivi: “Wakaanza kujadiliana kati yao kuhusu ni nani angekuwa mkuu zaidi kati yao.” Je, tunaweza pia kuanza kufikiri kwamba kwa njia fulani sisi ni bora kuliko waamini wenzetu au sisi ni bora kuliko watu wengine kwa ujumla? Watu wengi katika ulimwengu unaotuzunguka wanachochewa na kiburi na uchoyo. Acheni tuepuke kabisa kiburi kwa kutenda kwa unyenyekevu. Tukifanya hivyo na kutanguliza mapenzi ya Yehova, tutawaburudisha zaidi ndugu na dada zetu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki