Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
    • Ona kwamba Yesu alisema kuwa mtu huyo anapata anachohitaji “kwa sababu ya kudumu kwake kwa ujasiri.” (Luka 11:8) Maneno ‘kudumu kwa ujasiri’ yanapatikana mara moja tu katika Biblia. Yametafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki linalomaanisha kihalisi “kutoona haya.” Mara nyingi, kutoona haya ni sifa mbaya. Hata hivyo, mtu anapoendelea kuomba kitu kizuri bila kuacha au bila kuona haya, sifa hiyo inakuwa nzuri. Ndivyo alivyo yule mtu anayepata mgeni katika mfano huo. Haoni haya kuomba bila kuacha kile anachohitaji. Kwa kuwa Yesu anamtumia mtu huyo kama mfano kwetu, tunapaswa vivyo hivyo kusali bila kuacha. Yehova anataka ‘tuendelee kuomba, tuendelee kutafuta, tuendelee kupiga hodi.’ Na Yehova, ‘atawapa roho takatifu wale wanaomwomba.’

  • Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
    • Vivyo hivyo, Wakristo wa kweli wanaendelea kukabili hali ya hatari. Kwa kweli, Shetani anazunguka-zunguka kama “simba anayenguruma,” akijaribu kutumeza. (1 Petro 5:8) Ili tuendelee kuwa hai kiroho, ni lazima kabisa tupate msaada wa roho ya Mungu. Tusipomwomba Mungu msaada, tunaweza kupata msiba. Hivyo, kwa ujasiri tunaendelea bila kuacha kumwomba Mungu atupe roho yake takatifu. (Waefeso 3:14-16) Ni kwa kufanya hivyo tu ndipo tutaendelea kuwa na nguvu zinazohitajiwa ili ‘kuvumilia mpaka mwisho.’—Mathayo 10:22; 24:13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki