-
Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
Yesu aliuliza hivi: “Kwa kweli, ni baba gani kati yenu ambaye, ikiwa mwana wake anaomba samaki, labda atampa nyoka badala ya samaki? Au ikiwa pia anaomba yai, atampa nge?”
-
-
Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
12. Mfano wa baba anayekubali ombi la mwana wake unakazia namna gani utayari wa Yehova wa kujibu sala zetu?
12 Kupitia mfano wa jinsi baba anavyoitikia ombi la mwana wake, Yesu anafunua jinsi Yehova anavyohisi kuhusu wale wanaomfikia katika sala. (Luka 10:22) Kwanza, ona tofauti kati ya mifano hiyo miwili. Tofauti na mtu aliyetajwa katika mfano wa kwanza ambaye alisita kutoa msaada, Yehova ni kama mzazi wa kibinadamu anayejali, ambaye ana hamu ya kukubali ombi la mtoto wake. (Zaburi 50:15)
-
-
Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
14. (a) Watu fulani wanaokabili majaribu wanasumbuliwa na maoni gani yasiyofaa? (b) Tunapokabili majaribu, kwa nini tunaweza kusali kwa Yehova tukiwa na uhakika?
14 Mfano wa Yesu wa baba anayejali unakazia pia kwamba wema wa Yehova unapita kwa mbali wema wa mzazi yeyote wa kibinadamu. Kwa hiyo, hakuna yeyote kati yetu anayepaswa kuhisi kwamba majaribu ambayo huenda tunakabili yanaonyesha kuwa Mungu hapendezwi nasi. Adui yetu mkuu Shetani ndiye anayetaka tufikiri hivyo. (Ayubu 4:1, 7, 8; Yohana 8:44) Hakuna andiko linalosema kwamba tunapaswa kujilaumu. Yehova hatujaribu na “mambo maovu.” (Yakobo 1:13) Hatuletei majaribu kana kwamba anatupa nyoka au nge.
-