Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
    • “Alipokuwa angali mbali sana, baba yake alimwona mara hiyo naye akasukumwa na sikitiko, naye akakimbia akaangukia shingo yake na kumbusu kwa wororo.

  • “Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
    • —Luka 15:20-24.

  • “Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
    • 16 Mzazi yeyote mwenye upendo angetamani sana mtoto apate nguvu tena kiroho. Kwa sababu hiyo, twaweza tu kuwazia baba ya mwana mpotevu akitazama kila siku njia iliyokuwa mbele ya nyumba yake, akitumaini kwa hamu kurudi kwa mwana wake. Sasa amwona mwana wake njiani akija! Bila shaka sura ya mvulana huyo ilikuwa imebadilika. Hata hivyo, baba anamtambua alipokuwa “angali mbali sana.” Yeye anapuuza mavazi yaliyorarukararuka na hali ya kushuka moyo; yeye anamwona mwana wake, naye anakimbia kumlaki!

      17 Baba alipomfikia mwana wake, alimwangukia shingoni na kumbusu kwa wororo.

  • “Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
    • 18, 19. (a) Mfano wenye somo wa mwana mpotevu unakufunza nini kuhusu Yehova? (b) Yehova ‘hungojaje’ kurudi kwa mtenda-dhambi kama ionyeshwavyo na shughuli zake na Yuda na Yerusalemu?

      18 Kufikia hapo, mfano wenye somo wa mwana mpotevu hutufunza nini kuhusu Mungu ambaye tunapendelewa kumwabudu? Kwanza, tunajifunza kwamba Yehova “ni mwenye rehema na neema, asiye mwepesi wa hasira na mwingi wa fadhili-upendo na kweli.” (Kutoka 34:6, NW) Kwa kweli, rehema ni sifa kuu ya Mungu. Ni njia yake ya kawaida ya kuwaonyesha hisia walio na uhitaji. Basi, mfano wa Yesu wenye somo watufundisha kwamba Yehova yu “tayari kusamehe.” (Zaburi 86:5) Yeye yu macho, kusema kitamathali, ili kuona badiliko lolote la maoni ya wanadamu wenye dhambi ambalo lingemwandalia msingi wa kuonyesha rehema.—2 Mambo ya Nyakati 12:12; 16:9.

      19 Kwa kielelezo, fikiria shughuli za Mungu pamoja na Israeli. Nabii Isaya alipuliziwa na Yehova afafanue Yuda na Yerusalemu kuwa na ‘ugonjwa tangu kichwani hadi wayo wa mguu.’ Hata hivyo, yeye pia alisema: “BWANA atangoja, ili awaonee huruma, na kwa ajili ya hayo atatukuzwa, ili awarehemu.” (Isaya 1:5, 6; 30:18; 55:7; Ezekieli 33:11) Kama yule baba katika mfano wenye somo wa Yesu, Yehova ‘hutazama njia,’ kusema kitamathali. Anatazamia kwa hamu kurudi kwa wowote wale ambao wameacha nyumba yake. Je, tusingetarajia baba mwenye upendo afanye hivyo?—Zaburi 103:13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki