-
Mlo wa Jioni wa Bwana Una Maana Kubwa KwakoMnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 1
-
-
Alifanya vivyo hivyo na kikombe cha divai. Yesu alisema: “Kikombe hiki chamaanisha agano jipya kwa msingi wa damu yangu, ambayo yapasa kumwagwa kwa ajili yenu.”—Luka 22:20.
Katika masimulizi ya Mathayo, Yesu alisema hivi kuhusu kikombe: “Hii yamaanisha ‘damu yangu ya agano,’ inayopaswa kumwagwa kwa niaba ya wengi kwa msamaha wa dhambi.” (Mathayo 26:28) Yesu alitumia divai iliyokuwa ndani ya kikombe kama mfano wa damu yake. Damu yake iliyomwagwa ingekuwa msingi wa “agano jipya” kwa wanafunzi watiwa-mafuta, ambao wangetawala wakiwa wafalme na makuhani pamoja naye mbinguni.—Yeremia 31:31-33; Yohana 14:2, 3; 2 Wakorintho 5:5; Ufunuo 1:5, 6; 5:9, 10; 20:4, 6.
Divai iliyokuwa ndani ya kikombe inatukumbusha kwamba damu ya Yesu iliyomwagwa ingekuwa msingi wa “msamaha wa dhambi,” na hivyo kuwawezesha wale wanaoinywa kwenda mbinguni ili kuwa warithi pamoja na Kristo. Kama inavyotazamiwa, wale wanaopokea mwito huo wa kimbingu, ambao ni idadi ndogo, ndio pekee wanaokula mkate na kunywa divai kwenye Ukumbusho.—Luka 12:32; Waefeso 1:13, 14; Waebrania 9:22; 1 Petro 1:3, 4.
Namna gani wale wafuasi wengine wote wa Yesu ambao hawako katika agano jipya? Hawa ni “kondoo wengine” wa Bwana wanaotazamia kufurahia uhai wa milele katika paradiso duniani, wala si kutawala pamoja na Kristo mbinguni. (Yohana 10:16; Luka 23:43; Ufunuo 21:3, 4) “Umati mkubwa” wa Wakristo waaminifu “wanaomtolea Mungu utumishi mtakatifu mchana na usiku” wanafurahia kuwa watazamaji wenye shukrani kwenye Mlo wa Jioni wa Bwana. Kwa kweli, wao hutangaza hivi kwa maneno na matendo yao: “Sisi tunawiwa wokovu na Mungu wetu, aketiye juu ya hicho kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.”—Ufunuo 7:9, 10, 14, 15.
-
-
Mlo wa Jioni wa Bwana Una Maana Kubwa KwakoMnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 1
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 6]
“HUU NI MWILI WANGU” AU “HUU WAMAANISHA MWILI WANGU”?
Yesu aliposema, “mimi ndimi mlango” na, “mimi ndio mzabibu wa kweli,” hakuna aliyefikiria kwamba alikuwa mlango halisi au mzabibu halisi. (Yohana 10:7; 15:1) Vivyo hivyo, Biblia ya Union Version inapomnukuu Yesu kuwa anasema: “Kikombe hiki ni agano jipya,” hatukati kauli kwamba kikombe chenyewe kilikuwa kihalisi agano jipya. Hivyo pia, aliposema mkate ‘ulikuwa’ mwili wake, ni wazi kwamba mkate ulimaanisha au uliwakilisha mwili wake. Hivyo, tafsiri ya Biblia ya Charles B. Williams inasema: “Huu wawakilisha mwili wangu.”—Luka 22:19, 20.
-