-
Endeleeni Kutenda MemaMnara wa Mlinzi—2008 | Mei 15
-
-
5, 6. Kwa nini tunapaswa kuwapenda adui zetu?
5 Kwa nini tunapaswa kuwapenda adui zetu? Yesu alisema, “Ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni.” (Mt. 5:45) Tunapotii shauri hilo, tunakuwa “wana” wa Mungu kwa kumwiga Yehova, ambaye “hulichomoza jua lake juu ya watu waovu na wema na hunyesha mvua juu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.” Kama simulizi la Luka linavyoonyesha, Mungu “ni mwenye fadhili kuwaelekea wasio na shukrani na waovu.”—Luka 6:35.
-
-
Endeleeni Kutenda MemaMnara wa Mlinzi—2008 | Mei 15
-
-
2 Yesu Kristo aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Endeleeni kuwapenda adui zenu na kutenda mema.” (Luka 6:35) Acheni basi tuchunguze kwa makini himizo hilo. Pia, tutafaidika na mambo mengine ambayo Yesu alisema kuhusu kuwatendea wengine mema.
‘Muwapende Adui Zenu’
3. (a) Kwa maneno yako mwenyewe, eleza kwa ufupi maneno ya Yesu kwenye Mathayo 5:43-45. (b) Ni maoni gani kuhusu Wayahudi na watu wasio Wayahudi yaliyotokezwa na viongozi wa dini ya Kiyahudi wa karne ya kwanza?
3 Katika Mahubiri yake ya Mlimani yanayojulikana sana, Yesu aliwaambia wasikilizaji wake wawapende adui zao na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa. (Soma Mathayo 5:43-45.) Waliokuwepo katika pindi hiyo walikuwa Wayahudi, ambao waliijua amri hii ya Mungu: “Usilipize kisasi wala usiwe na kinyongo juu ya wana wa watu wako; nawe mpende mwenzako kama wewe mwenyewe.” (Law. 19:18) Viongozi wa dini ya Kiyahudi wa karne ya kwanza waliamini kwamba maneno “wana wa watu wako” na “mwenzako” yaliwahusu tu Wayahudi. Sheria ya Musa iliwataka Waisraeli wajitenge na mataifa mengine, lakini kulingana na maoni yaliyokuwepo wakati huo, watu ambao si Wayahudi walionwa kuwa maadui na kila mmoja wao alipaswa kuchukiwa.
4. Wanafunzi wa Yesu walipaswa kuwatendea adui zao jinsi gani?
4 Kinyume na hilo, Yesu alisema: “Endeleeni kuwapenda adui zenu na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa ninyi.” (Mt. 5:44) Wanafunzi wake walipaswa kuwatendea kwa upendo wale wote ambao waliwachukia. Kulingana na Luka, mwandikaji wa Injili, Yesu alisema hivi: “Mimi ninawaambia ninyi mnaosikiliza, Endeleeni kuwapenda adui zenu, kuwafanyia mema wale wanaowachukia, kuwabariki wale wanaowalaani, kusali kwa ajili ya wale wanaowatusi.” (Luka 6:27, 28) Kama watu wa karne ya kwanza ambao walifuata maneno ya Yesu, ‘tunawafanyia mema wale wanaotuchukia’ kwa kuwatendea kwa fadhili. ‘Tunawabariki wale wanaotulaani’ kwa kuzungumza nao kwa njia ya fadhili. Na ‘tunasali kwa ajili ya wale wanaotutesa’ kimwili au ‘wanaotutusi’ au kututesa kwa njia nyinginezo. Sala hizo zinaonyesha kwamba tunawapenda maadui wetu kwa sababu tunasali ili wabadili mioyo yao na kuchukua hatua ambayo itawaletea kibali cha Yehova.
5, 6. Kwa nini tunapaswa kuwapenda adui zetu?
5 Kwa nini tunapaswa kuwapenda adui zetu? Yesu alisema, “Ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni.” (Mt. 5:45) Tunapotii shauri hilo, tunakuwa “wana” wa Mungu kwa kumwiga Yehova, ambaye “hulichomoza jua lake juu ya watu waovu na wema na hunyesha mvua juu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.” Kama simulizi la Luka linavyoonyesha, Mungu “ni mwenye fadhili kuwaelekea wasio na shukrani na waovu.”—Luka 6:35.
-