-
Mungu na Kristo Wana Maoni Gani Kuhusu Wanawake?Amkeni!—2008 | Januari
-
-
Simulizi katika Injili ya Yohana linasema hivi: “Mwanamke mmoja wa Samaria akaja kuteka maji. Yesu akamwambia: ‘Nipe maji ninywe.’” Yesu alikuwa tayari kuzungumza na mwanamke Msamaria hadharani, hata ingawa Wayahudi wengi hawakuwa na shughuli na Wasamaria. Kulingana na The International Standard Bible Encyclopedia, kwa Wayahudi, “mazungumzo pamoja na mwanamke katika mahali pa hadharani lilikuwa jambo la kuchukiza hasa.” Hata hivyo, Yesu aliwatendea wanawake kwa heshima na ufikirio, naye hakuwabagua watu kwa sababu ya jamii au jinsia yao.
-