-
“Katika Hatari za Baharini”Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Ni jambo gani linaloweza kusemwa kuhusu meli iliyovunjikia Malta ambayo Paulo alikuwa amepanda? Ilikuwa meli ya nafaka, “mashua kutoka Aleksandria ikisafiri kuelekea Italia.” (Matendo 27:6, New World Translation of the Holy Scriptures—With References, kielezi-chini) Makundi ya meli za nafaka yalimilikiwa kibinafsi na Wagiriki, Wafoinike, na Wasiria, walioziongoza na kuziandalia vifaa. Hata hivyo, meli hizo zilikodiwa na Serikali. “Kama ilivyokuwa katika kukusanya kodi,” asema mwanahistoria William M. Ramsay, “serikali iliona kuwa ni rahisi kuwapa wanakandarasi kazi hiyo kuliko kujipangia watu na vifaa vingi sana vilivyohitajika kwa utumishi huo mkubwa.”
-
-
“Katika Hatari za Baharini”Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Roma pia lilitegemea biashara ya usafirishaji wa meli ili kupata chakula chake. Likiwa na watu wapatao milioni moja hivi, Roma lilikuwa na mahitaji makubwa mno ya nafaka—kati ya tani 250,000 na tani 400,000 kwa mwaka. Nafaka hiyo yote ilitoka wapi? Flavius Josephus amnukuu Herode Agripa wa Pili akisema kwamba Afrika Kaskazini ililisha Roma kwa miezi minane ya mwaka, ilhali Misri ilipeleka nafaka ya kutosha kutegemeza jiji hilo kwa miezi minne iliyobaki. Maelfu ya vyombo vya baharini yalitumiwa kupeleka chakula jijini humo.
-