-
“Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”Mnara wa Mlinzi—2009 | Oktoba 15
-
-
13, 14. (a) Kwa nini hatushangai tunapopata upinzani? (b) Tunaweza kuwabariki jinsi gani wale wanaotutesa?
13 Soma Waroma 12:14,
-
-
“Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”Mnara wa Mlinzi—2009 | Oktoba 15
-
-
14 Badala ya kuwachukia wale wanaotutesa, tunajitahidi kuwafundisha, huku tukitambua kwamba huenda wengine wao wanatenda hivyo kwa kutojua. (2 Kor. 4:4) Tunajitahidi kutii shauri hili la Paulo: “Endeleeni kuwabariki wale wanaowatesa; muwe mkibariki wala msiwe mkilaani.” (Rom. 12:14) Njia moja ya kuwabariki wapinzani wetu ni kusali kwa ajili yao. Yesu alisema hivi katika Mahubiri yake ya Mlimani: “Endeleeni kuwapenda adui zenu, kuwafanyia mema wale wanaowachukia, kuwabariki wale wanaowalaani, kusali kwa ajili ya wale wanaowatusi.” (Luka 6:27, 28) Mtume Paulo alijua kutokana na maisha yake mwenyewe kwamba mtesaji anaweza kugeuka na kuwa mwanafunzi mwaminifu wa Kristo na mtumishi mwenye bidii wa Yehova. (Gal. 1:13-16, 23) Katika barua nyingine, Paulo alisema: “Tunapotukanwa, tunabariki; tunapoteswa, tunavumilia; tunapoharibiwa sifa, tunasihi.”—1 Kor. 4:12, 13.
-