-
Mwigeni Yehova, Mungu Wetu Asiye na UbaguziMnara wa Mlinzi—2003 | Juni 15
-
-
11. Kutendea watu bila ubaguzi kulionyeshwaje katika kutaniko la kwanza la Kikristo?
11 Katika kutaniko la kwanza la Kikristo, Wayahudi na watu wa mataifa walikuwa sawasawa. Paulo alieleza hivi: “Utukufu na heshima na amani kwa kila mtu afanyaye lililo jema, kwa Myahudi kwanza na pia kwa Mgiriki. Kwa maana hakuna ubaguzi kwa Mungu.”b (Waroma 2:10, 11) Kile kilichoamua kama wangenufaika na fadhili zisizostahiliwa za Yehova, si asili yao, bali ni jinsi walivyotenda baada ya kujifunza kumhusu Yehova na matarajio yaliyotolewa na fidia ya Mwana wake Yesu. (Yohana 3:16, 36)
-