-
Mungu Anapendekeza Upendo Wake KwetuMnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
Lakini bado tunaweza kufarijiwa kwa kujua kwamba mwanamume mkamilifu, Yesu, angeweza kuleta matokeo yaliyo kinyume kabisa. Matokeo gani? Tunapata jibu katika maneno haya ya Paulo: “Kutangazwa [kwa watu wa namna zote] kuwa waadilifu kwa ajili ya uzima.”—Rom. 5:18.
9. Mungu alikuwa akifanya nini alipotangaza wanadamu kuwa waadilifu, kama inavyotajwa katika Waroma 5:16, 18?
9 Ni nini maana ya maneno ya Kigiriki yanayotafsiriwa kuwa “tangazo la uadilifu” na “kutangazwa kuwa waadilifu”? Mtafsiri mmoja wa Biblia aliandika hivi kuhusu wazo hilo: “Ni maneno ya mfano ya kisheria ambayo yanaonyesha jambo halali kisheria. Yanaonyesha badiliko la msimamo wa mtu mbele za Mungu, si badiliko linalofanyika ndani ya mtu . . . Maneno hayo ya mfano yanaonyesha kwamba Mungu ni hakimu au mwamuzi ambaye amefanya uamuzi ambao unampendelea mshtakiwa, ambaye ameletwa mbele ya mahakama ya Mungu, kwa njia ya mfano, akiwa ameshtakiwa kwa kosa la kutokuwa mwadilifu. Lakini Mungu anamwondolea mshtakiwa huyo hatia.”
-
-
Mungu Anapendekeza Upendo Wake KwetuMnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
14, 15. Ni thawabu gani ambayo wale wanaotangazwa na Mungu kuwa waadilifu waliahidiwa, lakini bado walihitaji kufanya nini?
14 Hebu fikiria zawadi kubwa ajabu kutoka kwa Mweza-Yote ya kusamehe dhambi ambazo mtu alirithi kutia ndani makosa aliyofanya! Huwezi kuhesabu dhambi ambazo watu mmoja-mmoja walitenda kabla ya kuwa Wakristo; hata hivyo, kwa msingi wa dhabihu ya ukombozi, Mungu anaweza kusamehe dhambi hizo. Paulo aliandika hivi: “Zawadi ilitokana na makosa mengi katika tangazo la uadilifu.” (Rom. 5:16) Mitume na watu wengine ambao walipokea zawadi hiyo yenye upendo (kutangazwa kuwa waadilifu) walipaswa kuendelea kumwabudu Mungu wa kweli wakiwa na imani.
-