-
Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na AmaniMnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
-
-
Waroma 8:1, 2.) Kupitia roho yake takatifu, Yehova anawafanya kuwa wana, na kuwaita kuwa “warithi pamoja na Kristo.” (Rom. 8:14-17) Roho ya Mungu, pamoja na imani yao katika fidia au dhabihu ya ukombozi ya Kristo, inawawezesha kuwa washindi katika pambano ambalo Paulo alieleza na hivyo “hawana hukumu ya hatia.” Wanawekwa huru kutokana na “sheria ya dhambi na kifo.”
-
-
Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na AmaniMnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
-
-
9. Neno “sheria” linalotumiwa katika Waroma 8:2 linamaanisha nini?
9 Zaidi ya “Sheria,” Paulo alitaja “sheria ya ile roho” na “sheria ya dhambi na kifo.” (Rom. 8:2) Hizo ni sheria gani? Neno “sheria” hapa halimaanishi amri fulani, kama zile zilizo katika Sheria ya Musa. Kitabu kimoja cha marejeo kinadokeza hivi: “Neno la Kigiriki linalotafsiriwa sheria katika mstari huo linamaanisha mambo mema au maovu ambayo watu wanafanya na ambayo yanawaongoza kama sheria. Neno hilo linaweza pia kumaanisha viwango ambavyo mtu anafuata maishani.”
10. Tunaongozwa jinsi gani na sheria ya dhambi na kifo?
10 Mtume Paulo aliandika hivi: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.” (Rom. 5:12) Tukiwa wazao wa Adamu, sisi sote tunaongozwa na sheria ya dhambi na kifo. Mwili wetu wenye dhambi unatuchochea sikuzote kufanya mambo yasiyompendeza Mungu, lakini mambo hayo yanaongoza tu kwenye kifo. Katika barua yake kwa Wagalatia, Paulo aliyaita matendo na tabia kama hizo kuwa “matendo ya mwili.” Kisha akaongeza hivi: “Wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Gal. 5:19-21) Watu wa aina hiyo ni sawa na wale wanaotembea kupatana na mwili. (Rom. 8:4) ‘Mambo yanayowaongoza’ na ‘viwango wanavyofuata maishani’ ni vya kimwili kabisa. Je, ni wale tu ambao wanafanya uasherati, kuabudu sanamu, kuwasiliana na pepo, au kutenda dhambi nyingine nzito ndio wanaotembea kupatana na mwili? Hapana, kwa kuwa matendo ya mwili yanatia ndani pia mambo ambayo huenda wengine wakayaona kuwa tu kasoro za utu, kama vile wivu, milipuko ya hasira, ugomvi, na kuwaonea wengine kijicho. Ni nani anayeweza kusema kwamba yeye ameacha kabisa kutembea kupatana na mwili?
11, 12. Ni uandalizi gani ambao Yehova amefanya ili kutusaidia kushinda sheria ya dhambi na kifo, na ni lazima tufanye nini ili tupate kibali cha Mungu?
11 Tunafurahi kama nini kwamba Yehova amefanya iwezekane kwetu kuishinda sheria hiyo ya dhambi na kifo! Yesu alisema hivi: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.” Kwa kukubali upendo wa Mungu na kuwa na imani katika dhabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo, tunaweza kuwekwa huru kutokana na hukumu ya dhambi tuliyorithi. (Yoh. 3:16-18) Kwa hiyo, huenda tukachochewa kusema hivi kama Paulo: “Shukrani kwa Mungu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu!”
-