-
Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na AmaniMnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
-
-
Paulo alionyesha kwamba kupitia roho ya Mungu na dhabihu ya ukombozi ya Mwana wake, Mungu ametimiza jambo fulani ambalo Sheria ya Musa haingeweza kutimiza.
8 Sheria, pamoja na amri zake nyingi, ziliwahukumu watenda-dhambi. Zaidi ya hayo, makuhani wakuu wa Israeli waliotumika chini ya Sheria hawakuwa wakamilifu na hawangeweza kutoa dhabihu ya kufunika dhambi kikamili. Hivyo, Sheria ilikuwa “dhaifu kupitia mwili.” Lakini “kwa kumtuma Mwana wake mwenyewe akiwa katika mfano wa mwili wenye dhambi” na kwa kumtoa kuwa dhabihu ya ukombozi, Mungu “aliihukumu dhambi katika mwili,” na hivyo kushinda tatizo la ‘Sheria kutokuwa na uwezo.’
-