-
Kusudi la Yehova LafanikiwaMwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
Uhuru Mzuri Ajabu Utakaokuwapo Wakati Ujao
11. Waokokaji wa dhiki kubwa watafurahia uhuru gani wa ajabu?
11 Dhiki kubwa iishapo wakati wa Har–Magedoni, uovu utakuwa umekomeshwa duniani, na Shetani Ibilisi hatakuwa tena “mungu wa huu mfumo wa mambo.” Waabudu wa Yehova hawatapambana tena na uvutano mwovu wa Shetani. (2 Wakorintho 4:4; Ufunuo 20:1, 2) Dini isiyo ya kweli haitamletea Yehova suto tena wala kuwagawanya wanadamu. Watumishi wa Mungu wa kweli hawatadhulumiwa wala kuteswa tena na mamlaka za wanadamu. Watafurahia uhuru mzuri ajabu!
12. Wanadamu wote watawekwaje huru kutoka katika dhambi na madhara yake?
12 Yesu, yule “Mwana-Kondoo wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi ya ulimwengu,” atafuta dhambi zote za wanadamu akitumia thamani ya dhabihu yake. (Yohana 1:29) Yesu alipokuwa duniani, aliwaponya watu kwa kuwasamehe dhambi zao. (Mathayo 9:1-7; 15:30, 31) Vivyo hivyo, Kristo Yesu, akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu huko mbinguni, atawaponya kimuujiza vipofu, mabubu, viziwi, walemavu, wenye ugonjwa wa akili, na wale wenye magonjwa mengine yoyote. (Ufunuo 21:3, 4) “Sheria ya dhambi” ambayo watu wote watiifu wanayo itafutiliwa mbali hivi kwamba mawazo na matendo yao yatakuwa yenye kupendeza kwao wenyewe na kwa Mungu. (Waroma 7:21-23) Mwishoni mwa Miaka Elfu Moja, wanadamu watakuwa wakamilifu, katika ‘sura na mfano’ wa Mungu wa pekee wa kweli.—Mwanzo 1:26.
13. Kristo atafanya nini mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu Moja, na matokeo yatakuwa nini?
13 Baada ya Kristo kuwasaidia wanadamu wote kuwa wakamilifu, atamrudishia Baba yake mamlaka aliyokabidhiwa ili kutimiza kazi hiyo: ‘Atamkabidhi ufalme Mungu wake aliye Baba, wakati akiwa amefanya serikali yote na mamlaka yote na nguvu kuwa si kitu. Kwa maana ni lazima yeye atawale akiwa mfalme mpaka Mungu awe ameweka maadui wote chini ya miguu yake.’ (1 Wakorintho 15:24, 25) Utawala wa Ufalme wa Miaka Elfu Moja utakuwa umetimiza kusudi lake kwa ukamili; basi hakutakuwa na uhitaji tena wa serikali hiyo saidizi kuwapatanisha watu pamoja na Yehova. Jukumu la Yesu akiwa Mkombozi litakoma kwa kuwa wanadamu watakuwa wamekombolewa, dhambi na kifo vitakuwa vimekomeshwa kabisa. Biblia yaeleza hivi: “Ndipo Mwana mwenyewe atakapojitiisha pia kwa Yule aliyetiisha vitu vyote kwake, ili Mungu apate kuwa vitu vyote kwa kila mtu.”—1 Wakorintho 15:28.
14. Wanadamu wote wakamilifu watapatwa nini, na kwa nini?
14 Kisha, wanadamu hao wakamilifu watapewa nafasi ya kuonyesha kwamba wameamua kumtumikia Mungu wa pekee wa kweli milele. Kwa hiyo, kabla ya kuwakubali kabisa kuwa watoto wake, Yehova atawaacha wanadamu hao wakamilifu wapate jaribu la mwisho. Shetani na mashetani wake watafunguliwa kutoka katika abiso. Wale wanaompenda Yehova kwelikweli hawatapata madhara ya kudumu. Lakini watu wasio waaminifu ambao watashawishiwa wamwasi Yehova wataangamizwa milele, pamoja na yule mwasi wa awali na mashetani wake.—Ufunuo 20:7-10.
15. Malaika na wanadamu wote watakuwa katika hali gani tena?
15 Kisha Yehova atawakubali wanadamu wote wakamilifu ambao waliunga mkono haki yake ya kutawala wakati wa jaribu la mwisho, kuwa watoto wake. Ndipo watakapofurahia kikamili uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu wakiwa washiriki wa familia ya Mungu ya ulimwenguni pote.
-
-
Kusudi la Yehova LafanikiwaMwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
9. Andiko la Waroma 8:21 linawaahidi nini wanadamu?
9 Watu hao wenye tumaini la kuishi duniani wanasubiri kwa hamu wakati ambapo wanadamu wote ‘watawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu.’ (Waroma 8:21) Wataanza kuwekwa huru baada ya Kristo na majeshi yake ya mbinguni kukomesha dhiki kubwa wakati wa Har–Magedoni. Ulimwengu wote mwovu wa Shetani utaharibiwa wakati huo, halafu Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja utaleta baraka.—Ufunuo 19:17-21; 20:6.
-