-
WanawakeKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kila mwanamke ambaye husali au kutoa unabii kichwa chake kikiwa hakijafunikwa hukiaibisha kichwa chake
-
-
WanawakeKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
(Mwanamke Mkristo anapofunika kichwa katika pindi zinazofaa, jambo hilo huonyesha kwamba yeye anaheshimu mpango wa ukichwa ulioanzishwa na Mungu. Kristo huheshimu ukichwa wa kitheokrasi; mwanamume na mwanamke pia wana wajibu wa kufanya hivyo.
-
-
WanawakeKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Hata hivyo, mwanamke ‘kusali au kutoa unabii’ bila kufunika kichwa kungeonyesha ukosefu wa heshima kwa cheo cha mwanamume alichopewa na Mungu na kungemwaibisha.
-
-
WanawakeKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ni wakati gani inapokuwa lazima kwa mwanamke kufunika kichwa?
Wakati ‘anaposali au kutoa unabii,’ kama ilivyoandikwa katika 1 Wakorintho 11:5. Hilo halimaanishi kwamba anahitaji kufunika kichwa wakati anaposali faraghani au anapoongea na wengine juu ya unabii wa Biblia. Hata hivyo, anapaswa kufunika kichwa kama ishara ya nje ya kuheshimu ukichwa wa mwanamume wakati mwanamke huyo anaposhughulikia mambo yanayohusu ibada ambayo kwa kawaida yangeshughulikiwa na mume wake au na mwanamume mwingine. Akisali kwa sauti kubwa kwa ajili yake mwenyewe au kwa ajili ya wengine au akiongoza funzo rasmi la Biblia, hivyo akifanya kazi ya kufundisha, mume wake akiwapo, anapaswa kufunika kichwa hata ikiwa mume hashiriki imani yake. Lakini kwa kuwa Mungu amemruhusu kuwafundisha watoto wake, hahitajiki kujifunika kichwa anaposali au anapojifunza pamoja na watoto wake wachanga ambao hawajajiweka wakfu wakati mume wake hayupo. Ikiwa, katika hali za pekee, mshiriki wa kiume wa kutaniko ambaye amejiweka wakfu yupo au wakati mwanamke huyo anapoandamana na mwangalizi asafiriye anapotembelea kutaniko, ndipo, wakati anapoongoza funzo la Biblia lililopangwa mapema, mwanamke huyo anapaswa afunike kichwa chake, lakini mwanamume huyo anapaswa atoe sala.
-