Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi Kamwe
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
    • 1 Wakorintho 13:4-

  • Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi Kamwe
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
    • Kazia fikira hasa sentensi ya mwisho ya mstari wa 7

  • Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi Kamwe
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
    • ‘Upendo huvumilia mambo yote.

  • Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi Kamwe
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
    • Upendo Unavumilia Mambo Yote

      14, 15. (a) Upendo unaweza kutusaidia jinsi gani kuvumilia majaribu? (b) Kwa nini ndugu mmoja kijana alikataa kulegeza msimamo wake?

      14 Ni nini kinachowawezesha Wakristo kuvumilia hata wanapokabili majaribu, hali ngumu, na matatizo yoyote yale? Hasa ni upendo ambao unategemea kanuni. Upendo huo unapita nguvu za kuachana tu na vitu vyetu vya kimwili. Unatuchochea kufikia hatua ya kuwa tayari kudumisha utimilifu wetu na hata kupoteza uhai wetu kwa ajili ya Kristo. (Luka 9:24, 25) Tafakari juu ya uaminifu wa Mashahidi walioteseka katika kambi za mateso, kambi za kazi ngumu, na katika magereza wakati na baada ya Vita vya Pili vya Ulimwengu.

      15 Mfano wa kijana mmoja Shahidi Mjerumani anayeitwa Wilhelm unaonyesha hilo. Badala ya kulegeza msimamo wake, alibaki mshikamanifu alipokuwa akingoja kuuawa kwa kupigwa risasi na kikundi cha askari wa Nazi. Katika barua ya kuaga familia yake, aliandika hivi: “Zaidi ya mambo yote tunapaswa kumpenda Mungu, kama Kiongozi wetu Yesu Kristo alivyoamuru. Tukisimama imara upande wa Mungu, atatuthawabisha.” Baadaye, katika gazeti moja la Mnara wa Mlinzi, mtu mmoja wa familia ya Wilhelm aliandika hivi: “Katika hali zenye misukosuko, sikuzote tumehakikisha kwamba tukiwa familia tunatanguliza upendo wetu kwa Mungu.” Na huo ndio mtazamo wa ndugu wengi ambao kwa sasa wanavumilia vifungo gerezani huko Armenia, Eritrea, Korea Kusini, na nchi nyinginezo. Ndugu hao wanaendelea kuwa imara katika upendo wao kwa Yehova.

      16. Ndugu zetu nchini Malawi walivumilia mateso gani?

      16 Katika maeneo mengi, majaribu ya aina mbalimbali yanajaribu imani na uvumilivu wa ndugu zetu. Kwa miaka 26, Mashahidi wa Yehova nchini Malawi walivumilia marufuku ya serikali, upinzani mkali, na ukatili mwingi. Walibarikiwa kwa sababu ya uvumilivu wao. Mateso yalipoanza, kulikuwa na Mashahidi 18,000 hivi katika nchi hiyo. Miaka 30 baadaye hesabu yao iliongezeka zaidi ya mara mbili kufikia 38,393. Matokeo kama hayo yameonekana katika nchi nyingine.

      17. Mashahidi fulani wanakabili hali gani katika familia zilizogawanyika kidini, na kwa nini wanavumilia mateso?

      17 Ingawa mashambulizi ya moja kwa moja kuelekea watu wa Mungu kwa ujumla yanaweza kuwa makali, hali inakuwa tofauti kabisa wakati Mkristo mmoja-mmoja anapopingwa na watu wa familia yake. Huenda tukapata mikazo kutoka kwa washiriki wa familia au watu wa karibu wa ukoo. Je, Yesu hakutabiri kwamba mambo hayo yangetukia? Ndiyo, na watu wengi wamejionea ukweli wa maneno yake. (Mt. 10:35, 36) Vijana fulani wamevumilia upinzani kutoka kwa wazazi wasio waamini. Wengine hata wamefukuzwa kutoka nyumbani, lakini wamekaribishwa na Mashahidi wenye fadhili. Wengine wamekataliwa na familia zao. Ni nini kilichowawezesha Mashahidi hao kuvumilia mateso? Si kwa sababu tu wanawapenda ndugu zao, bali kwa sababu hasa wanampenda kikweli Yehova na Mwana wake.—1 Pet. 1:22; 1 Yoh. 4:21.

      18. Upendo ambao unavumilia mambo yote unawasaidia jinsi gani Wakristo waliofunga ndoa?

      18 Tunahitaji pia kuonyesha upendo ambao unavumilia mambo yote tunapokabili hali nyingine nyingi maishani. Katika kifungo cha ndoa, upendo unawawezesha wenzi wa ndoa kuheshimu maneno haya ya Yesu: “Kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.” (Mt. 19:6) Wanapopatwa na “dhiki katika mwili wao,” Wakristo waliofunga ndoa wanapaswa kujikumbusha kwamba Yehova ni mtu muhimu sana katika ndoa yao. (1 Kor. 7:28) Neno lake linasema kwamba ‘upendo huvumilia mambo yote,’ na mume na mke ambao wanajivika sifa hiyo wanapata nguvu za kushikamana pamoja na kudumisha ndoa yao.—Kol. 3:14.

      19. Watu wa Mungu wamefanya nini baada ya misiba ya asili?

      19 Upendo unatusaidia kuvumilia mambo yote wakati wa misiba ya asili. Ndivyo ilivyokuwa wakati tetemeko la nchi lilipotikisa eneo la kusini la Peru na Kimbunga Katrina kilipoharibu sehemu fulani za eneo la Ghuba huko Marekani. Ndugu zetu wengi walipoteza nyumba zao au mali zao katika misiba hiyo. Upendo ulichochea kutaniko la ulimwenguni pote kuandaa misaada, na wajitoleaji walisaidia kujenga upya nyumba na kurekebisha Majumba ya Ufalme. Matendo kama hayo yanathibitisha kwamba ndugu zetu wanapendana na wanawajali wenzao nyakati zote na chini ya hali yoyote ile.—Yoh. 13:34, 35; 1 Pet. 2:17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki