Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • 5. Ni nani aliye msingi wa kutaniko la Kikristo, na hilo lilitabiriwaje?

      5 Paulo aliandika hivi: “Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine wowote zaidi kuliko uliowekwa, ambao ni Yesu Kristo.” (1 Wakorintho 3:11) Hii haikuwa mara ya kwanza ambayo Yesu alilinganishwa na msingi. Kwa kweli, andiko la Isaya 28:16 lilitabiri hivi: “Bwana, MUNGU, asema hivi, Tazama, naweka jiwe katika Sayuni, liwe msingi, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni lenye thamani, msingi ulio imara.” Kwa muda mrefu Yehova alikuwa amekusudia Mwana wake awe msingi wa kutaniko la Kikristo.—Zaburi 118:22; Waefeso 2:19-22; 1 Petro 2:4-6.

      6. Paulo aliwekaje msingi ufaao katika Wakristo Wakorintho?

      6 Ni nini ulio msingi wa Wakristo mmoja-mmoja? Kama Paulo alivyosema, msingi pekee wa Mkristo wa kweli ni ule uliowekwa na Neno la Mungu—Yesu Kristo. Bila shaka Paulo aliweka msingi kama huo. Huko Korintho, ambako falsafa zilistahiwa sana, hakujaribu kuwavutia watu kwa hekima ya kilimwengu. Badala ya hivyo, Paulo alihubiri “Kristo aliyetundikwa mtini,” jambo lililopuuzwa na mataifa kuwa “upumbavu” mkubwa. (1 Wakorintho 1:23) Paulo alifundisha kwamba Yesu ndiye mtu mwenye fungu kubwa zaidi katika makusudi ya Yehova.—2 Wakorintho 1:20; Wakolosai 2:2, 3.

  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • 8. Tunamwekaje Kristo awe msingi katika wale wanaotazamiwa kuwa wanafunzi?

      8 Tunapomweka Kristo awe msingi, hatumwasilishi akiwa mtoto mchanga katika hori, wala akiwa sawa na Yehova katika Utatu. La, maoni hayo yasiyo ya Kimaandiko ndiyo msingi wa Wakristo bandia. Badala ya hivyo, sisi hufundisha kwamba Yesu alikuwa mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi, kwamba alitoa uhai wake mkamilifu kwa niaba yetu, na kwamba leo yeye ni Mfalme aliyewekwa wa Yehova anayetawala mbinguni. (Waroma 5:8; Ufunuo 11:15) Sisi pia hujitahidi kuwachochea wanafunzi wetu wafuate hatua za Yesu na kuiga sifa zake. (1 Petro 2:21) Twataka wachochewe sana na bidii ya Yesu kwa ajili ya huduma, huruma yake kwa watu wa hali ya chini na wenye kuonewa, rehema yake kwa watenda-dhambi waliopondeka kutokana na hatia yao wenyewe, ujasiri wake usioyumbayumba alipokabili majaribu. Kwa kweli, Yesu ni msingi bora kabisa. Lakini ni nini kinachofuata?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki