Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • Kujenga kwa Vifaa Vifaavyo

      9. Ingawa kimsingi Paulo alikuwa mweka-msingi, yeye alikuwa na hangaiko lipi kuhusu wale waliokubali ukweli wa yale aliyofundisha?

      9 Paulo aliandika: “Basi yeyote akijenga juu ya huo msingi, dhahabu, fedha, mawe yenye bei, vifaa vya mbao, nyasi kavu, mabua, kazi ya kila mmoja itakuwa dhahiri, kwa maana ile siku itaifichua, kwa sababu itafunuliwa kwa njia ya moto; na moto wenyewe utathibitisha ni ya namna gani kazi ya kila mmoja.” (1 Wakorintho 3:12, 13) Paulo alimaanisha nini? Fikiria hali ya wakati huo. Kimsingi Paulo alikuwa mweka-msingi. Katika safari zake za umishonari, alisafiri kutoka jiji hadi jiji, akihubiria wengi ambao hawakuwa wamesikia kamwe juu ya Kristo. (Waroma 15:20) Watu walipokubali kweli aliyofundisha, makutaniko yalifanyizwa. Paulo aliwajali sana waaminifu hao. (2 Wakorintho 11:28, 29) Hata hivyo, kazi yake ilimtaka aendelee kusafiri. Kwa hiyo, baada ya kutumia miezi 18 akiweka msingi huko Korintho, aliondoka kwenda kuhubiri katika majiji mengine. Hata hivyo, alipendezwa sana na jinsi wengine walivyoendeleza kazi aliyokuwa amefanya huko.—Matendo 18:8-11; 1 Wakorintho 3:6.

      10, 11. (a) Paulo alitofautishaje aina mbalimbali za vifaa vya ujenzi? (b) Ni yapi yaliyokuwa majengo halisi ambayo yamkini yalikuweko katika Korintho la kale? (c) Ni majengo ya aina gani ambayo yaelekea zaidi kustahimili moto, nayo yaandaa kielelezo gani chenye funzo kwa wafanya-wanafunzi Wakristo?

      10 Yaonekana kwamba watu fulani waliokuwa wakijenga juu ya msingi ambao Paulo alikuwa ameweka huko Korintho hawakuwa wakifanya kazi nzuri. Ili kufichua tatizo hilo, Paulo atofautisha aina mbili za vifaa vya ujenzi: dhahabu, fedha, na mawe yenye bei; halafu vifaa vya mbao, nyasi kavu, na mabua. Jengo laweza kujengwa kwa vifaa bora, vyenye kudumu, visivyoweza kushika moto; au laweza kujengwa haraka-haraka kwa vifaa vya muda visivyoweza kutumika tena, na viwezavyo kushika moto kwa urahisi. Hapana shaka kwamba jiji kubwa kama Korintho lilikuwa na majengo mengi ya aina hizo mbili. Kulikuwa na mahekalu ya kuvutia yaliyojengwa kwa mawe yenye bei, labda sehemu fulani za hayo zikiwa zimefunikwa au kupambwa kwa dhahabu au fedha.b Labda majengo hayo yenye kudumu yalikuwa marefu na yenye fahari kushinda nyumba zilizokuwa karibu, vibanda na viduka vya sokoni vilivyojengwa kwa mbao zisizo laini na kuezekwa kwa nyasi.

  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • 12. Wakristo Wakorintho walikuwa wakifanyaje kiholela kazi ya kujenga?

      12 Kwa wazi, Paulo alihisi kwamba Wakristo katika Korintho walikuwa wakijenga vibaya. Kasoro ilikuwa nini? Kama vile muktadha uonyeshavyo, kutaniko hilo lilikuwa limekumbwa na mgawanyiko, kuvutiwa na watu mashuhuri kujapohatarisha umoja wa kutaniko. Baadhi yao walikuwa wakisema, “Mimi ni wa Paulo,” ilhali wengine walisisitiza, “Mimi ni wa Apolo.” Yaonekana wengine walijivunia mno hekima yao wenyewe. Si ajabu kwamba matokeo yalikuwa hali ya kufikiri kimwili, kutokomaa kiroho, na “wivu na zogo” iliyoenea sana. (1 Wakorintho 1:12; 3:1-4, 18) Bila shaka mitazamo hiyo ilidhihirika katika mafundisho yaliyofanywa kutanikoni na hudumani. Matokeo yalikuwa kwamba kazi yao ya kufanya wanafunzi ilifanywa kiholela, kama kazi ya kujenga iliyofanywa kwa vifaa duni. Haingeokoka “moto.” Paulo alikuwa akizungumzia moto upi?

  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • Jenga kwa vifaa vidumuvyo! Tukiwafundisha wanafunzi wetu ili kuwafikia mioyo, tukiwachochea wathamini sifa za Kikristo kama vile hekima, ufahamu, kumhofu Yehova, na imani ya kweli, basi tunajenga kwa vifaa vyenye kudumu, visivyoweza kushika moto. (Zaburi 19:9, 10; Mithali 3:13-15; 1 Petro 1:6, 7) Wanaojipatia sifa hizo wataendelea kufanya mapenzi ya Mungu; nao wana tumaini hakika la kuendelea kuwa hai milele. (1 Yohana 2:17) Ingawa hivyo, tunaweza kutumiaje kielezi hicho cha Paulo kwa njia ifaayo? Fikiria vielelezo kadhaa.

      15. Ni katika njia zipi tunaweza kuhakikisha kwamba tunaepuka kufanya kiholela kazi ya kujenga kuhusiana na wanafunzi wetu wa Biblia?

      15 Tunapowafundisha wanafunzi wa Biblia, hatupaswi kukuza wanadamu zaidi kushinda Yehova Mungu. Mradi wetu si kuwafundisha kutuona sisi kuwa chanzo kikuu cha hekima. Twataka wamtegemee Yehova, Neno lake, na tengenezo lake ili wapate mwongozo. Ili kufikia mradi huo, hatutajibu maswali yao kwa kutoa maoni yetu tu. Badala ya hivyo, tunawafundisha kutafuta majibu, wakitumia Biblia na vichapo ambavyo “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ameandaa. (Mathayo 24:45-47) Kwa sababu sawa na hizo, tunakuwa waangalifu tusiwe wenye kumiliki wanafunzi wetu wa Biblia. Badala ya kuona uchungu wengine wanapoonyesha kupendezwa nao, yatupasa tuwatie wanafunzi wetu moyo ‘wapanuke’ katika shauku zao nyororo na kupata kuwajua na kuwathamini watu wengi iwezekanavyo kutanikoni.—2 Wakorintho 6:12, 13.

      16. Wazee wanaweza kujengaje kwa vifaa visivyoweza kushika moto?

      16 Wazee Wakristo pia hutimiza fungu muhimu katika kujenga wanafunzi. Wanapofundisha mbele ya kutaniko, wao hujaribu kujenga kwa vifaa visivyoweza kushika moto. Huenda uwezo wao wa kufundisha, uzoefu, na utu wao ukatofautiana sana, lakini hawajinufaishi kwa kutumia tofauti hizi ili wajipatie wafuasi. (Linganisha Matendo 20:29, 30.) Hatujui ni kwa nini hasa wengine katika Korintho walikuwa wakisema, “Mimi ni wa Paulo” au, “Mimi ni wa Apolo.” Lakini twaweza kuwa na hakika kabisa kwamba hakuna yeyote wa wazee hawa waaminifu aliyeendeleza maoni kama hayo yenye kugawanya. Paulo hakufurahishwa na maoni hayo; aliyapinga kwa nguvu. (1 Wakorintho 3:5-7) Vivyo hivyo leo, wazee hukumbuka kwamba wao huchunga “kundi la Mungu.” (1 Petro 5:2) Kundi hilo si la mwanadamu yeyote. Kwa hiyo, wazee husimama imara dhidi ya mwelekeo wowote wa mtu mmoja kutawala ama kundi ama baraza la wazee. Maadamu wazee wanachochewa na tamaa yenye unyenyekevu ya kutumikia kutaniko, kufikia mioyo, na kusaidia kondoo wamtumikie Yehova kwa nafsi yote, wao hujenga kwa vifaa visivyoweza kushika moto.

      17. Wazazi Wakristo hujitahidije kujenga kwa vifaa visivyoweza kushika moto?

      17 Wazazi Wakristo pia huhangaikia sana jambo hilo. Wana tamaa kubwa kama nini ya kuona watoto wao wakiishi milele! Hiyo ndiyo sababu wao hujitahidi sana ili ‘kukaza kikiki’ kanuni za Neno la Mungu katika mioyo ya watoto wao. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7, NW) Wanataka watoto wao wajue kweli, si ikiwa fungu la sheria au mambo ya kukariri tu, bali ikiwa njia ya maisha iliyo kamili, yenye kuthawabisha, na yenye furaha. (1 Timotheo 1:11) Ili kuwajenga watoto wao wawe wanafunzi waaminifu wa Kristo, wazazi wenye upendo hujitahidi kutumia vifaa visivyoweza kushika moto. Kwa subira wao hufanya kazi pamoja na watoto wao, wakiwasaidia waache sifa ambazo Yehova huchukia na kusitawisha zile ambazo yeye hupenda.—Wagalatia 5:22, 23.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki