Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Hekima I Pamoja na Wenye Kiasi”
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 1
    • Paulo—Mtu ‘wa Chini’ na ‘Msimamizi-Nyumba’

      4. Paulo alipata mapendeleo gani ya kipekee?

      4 Paulo alikuwa mashuhuri miongoni mwa Wakristo wa mapema, na kwa sababu nzuri. Katika huduma yake, alisafiri maelfu ya kilometa baharini na barani, na alianzisha makutaniko mengi. Na zaidi, Yehova alimbariki Paulo kwa kumpa maono na uwezo wa kusema lugha za kigeni. (1 Wakorintho 14:18; 2 Wakorintho 12:1-5) Pia Yehova alimpulizia Paulo aandike barua 14 ambazo sasa ni sehemu ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kwa wazi, inaweza kusemwa kwamba kazi za Paulo zilizidi kazi za wale mitume wengine.—1 Wakorintho 15:10.

      5. Paulo alionyeshaje kwamba alikuwa na maoni yenye kiasi juu yake mwenyewe?

      5 Kwa kuwa Paulo alikuwa katika mstari wa mbele katika utendaji wa Kikristo, huenda wengine wangetarajia kumwona akifurahia kutukuzwa, hata akiringia mamlaka yake. Lakini, haikuwa hivyo, kwa kuwa Paulo alikuwa mwenye kiasi. Alijiita “mdogo zaidi sana kati ya wale mitume,” akiongezea: “Nami sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililinyanyasa kutaniko la Mungu.” (1 Wakorintho 15:9) Kwa kuwa aliwanyanyasa Wakristo zamani, Paulo hakusahau kamwe kwamba ni kupitia tu fadhili isiyostahiliwa ya Mungu angeweza kuwa na uhusiano na Mungu, sembuse kufurahia mapendeleo ya kipekee ya utumishi. (Yohana 6:44; Waefeso 2:8) Kwa hiyo, Paulo hakuhisi kwamba mafanikio yake ya ajabu katika huduma yalimfanya awe bora kuliko wengine.—1 Wakorintho 9:16.

      6. Paulo alionyeshaje kiasi aliposhughulika na Wakorintho?

      6 Jinsi Paulo alivyoshughulika na Wakorintho inadhihirisha sana kwamba alikuwa mwenye kiasi. Inaonekana kwamba baadhi yao walivutiwa na wale ambao walifikiri kuwa waangalizi mashuhuri, kutia ndani Apolo, Kefa, na Paulo mwenyewe. (1 Wakorintho 1:11-15) Lakini Paulo hakutafuta sifa kwa Wakorintho wala hakutumia vibaya heshima aliyopewa na wengine. Alipowazuru, yeye hakujitokeza ‘na usemi wenye kupita kiasi wala hekima.’ Badala yake, Paulo alisema hivi juu yake mwenyewe na waandamani wake: “Acheni mtu atukadirie sisi hivyo kama walio chini ya Kristo na wasimamizi-nyumba wa siri takatifu za Mungu.”a—1 Wakorintho 2:1-5; 4:1.

      7. Paulo alionyeshaje kiasi hata alipokuwa akitoa ushauri?

      7 Paulo hata alionyesha kiasi alipolazimika kutoa ushauri mkali na mwongozo. Badala ya kutumia mamlaka yake akiwa mtume, Paulo aliwasihi Wakristo wenzake “kwa huruma za Mungu” na “Msingi wa upendo.” (Waroma 12:1, 2; Filemoni 8, 9) Kwa nini Paulo alifanya hivyo? Kwa sababu kwa kweli alijiona kuwa ‘mfanyakazi mwenzi’ wa ndugu zake, wala hakujiona kuwa ‘bwana-mkubwa juu ya imani yao.’ (2 Wakorintho 1:24) Inaelekea kwamba sifa ya Paulo ya kiasi ndiyo iliyomfanya apendwe sana na makutaniko ya karne ya kwanza.—Matendo 20:36-38.

  • “Hekima I Pamoja na Wenye Kiasi”
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 1
    • a Neno la Kigiriki lililotafsiriwa “walio chini” linaweza kurejezea mtumwa ambaye alipiga makasia katika sehemu ya chini ya meli kubwa. Kwa kutofautisha, huenda “wasimamizi-nyumba” wakakabidhiwa mapendeleo zaidi, labda ya kutunza nyumba nyingi. Hata hivyo, machoni pa wakubwa wengi, msimamizi-nyumba alipaswa kuwa mtiifu kama tu mtumwa mwenye kupiga makasia katika sehemu ya chini ya meli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki