Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kushinda Udhaifu wa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 15
    • Hakuna kishawishi ambacho kimewapata nyinyi ila kilicho kawaida kwa watu. Lakini Mungu ni mwaminifu, naye hatawaacha nyinyi mshawishwe kupita vile mwezavyo kuhimili, bali pamoja na hicho kishawishi ataifanya pia njia ya kutokea kusudi mweze kuvumilia hilo.” (1 Wakorintho 10:12, 13) Sisi sote—vijana kwa wazee, wanaume kwa wanawake—hukabili vishawishi vingi shuleni, kazini, au kwingineko.

  • Kushinda Udhaifu wa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 15
    • 7. Kwa nini inafariji kujua kwamba wengine wamefaulu kukinza kishawishi?

      7 Tunapata faraja iliyoje kutokana na maneno ya Paulo: “Hakuna kishawishi ambacho kimewapata nyinyi ila kilicho kawaida kwa watu”! (1 Wakorintho 10:13) Mtume Petro aliandika: “Chukueni msimamo wenu dhidi ya [Ibilisi], mkiwa thabiti katika imani, mkijua kwamba mambo yaleyale kwa njia ya mateso yanatimizwa katika ushirika mzima wa ndugu zenu katika ulimwengu.” (1 Petro 5:9) Naam, wengine wamekabili vishawishi kama hivyo na kwa msaada wa Mungu wamefaulu kuvikinza, nasi pia twaweza kufanya hivyo. Hata hivyo, tukiwa Wakristo wa kweli tunaoishi katika ulimwengu uliopotoka, sote tunaweza kutarajia kushawishiwa siku moja.

  • Kushinda Udhaifu wa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 15
    • 12. Tunamwomba Mungu nini tunaposali: “Usituingize katika kishawishi”?

      12 Paulo atoa uhakikisho huu wenye kutia moyo: “Mungu ni mwaminifu, naye hatawaacha nyinyi mshawishwe kupita vile mwezavyo kuhimili, bali pamoja na hicho kishawishi ataifanya pia njia ya kutokea kusudi mweze kuvumilia hilo.” (1 Wakorintho 10:13) Njia moja ambayo Yehova hutusaidia ni kwa kujibu sala zetu za kupata msaada wake wa kupambana na kishawishi. Yesu Kristo alitufundisha kusali hivi: “Usituingize katika kishawishi, bali utukomboe kutokana na yule mwovu.” (Mathayo 6:13) Kwa kujibu sala hiyo ya kutoka moyoni, Yehova hatatuacha tushawishiwe; atatukomboa kutoka kwa Shetani na vitendo vyake vya hila. (Waefeso 6:11, NW, kielezi-chini) Yatupasa kumwomba Mungu atusaidie kutambua vishawishi na kuwa na nguvu za kuvikinza. Tukimsihi asiruhusu tushindwe tunaposhawishiwa, atatusaidia tusidanganywe na “yule mwovu,” Shetani.

      13. Tunapaswa kufanya nini tunapokabili kishawishi chenye kuendelea?

      13 Tunahitaji hasa kusali kwa bidii tunapokabili kishawishi chenye kuendelea. Vishawishi vingine vinaweza kutokeza mapambano makali sana ya akili, tukipambana na mawazo na mitazamo ambayo hutukumbusha kwa njia yenye kutokeza jinsi tulivyo dhaifu. (Zaburi 51:5) Kwa mfano, twaweza kufanya nini ikiwa tunasumbuliwa na kumbukumbu za zoea fulani potovu la zamani? Namna gani ikiwa tunashawishiwa kulirudia? Badala ya kujaribu tu kuzuia hisia hizo, mjulishe Yehova jambo hilo kupitia sala—tena na tena ikihitajika. (Zaburi 55:22) Kwa nguvu za Neno lake na roho yake takatifu, anaweza kutusaidia kuondoa maelekeo yasiyo safi akilini mwetu.—Zaburi 19:8, 9.

      14. Kwa nini sala ni muhimu ili kukabiliana na kishawishi?

      14 Alipoona mitume wake wakisinzia katika bustani ya Gethsemane, Yesu aliwasihi: “Fulizeni kulinda na kusali kwa kuendelea, ili msipate kuingia ndani ya jaribu. Bila shaka, roho ni yenye hamu, lakini mwili ni dhaifu.” (Mathayo 26:41) Njia moja ya kushinda kishawishi ni kuwa macho kutambua njia mbalimbali ambazo kishawishi kinaweza kutokea na kujua njia zake zenye hila. Ni muhimu pia kusali bila kukawia kuhusu kishawishi hicho ili tuweze kuwa tayari kiroho kupambana nacho. Kwa kuwa kishawishi hutushambulia sehemu ambazo sisi ni dhaifu zaidi, hatuwezi kukikinza peke yetu. Sala ni muhimu kwa sababu nguvu ambazo Mungu hutoa zaweza kutegemeza kinga yetu dhidi ya Shetani. (Wafilipi 4:6, 7) Huenda pia tukahitaji usaidizi wa kiroho na sala za “wanaume wazee wa kutaniko.”—Yakobo 5:13-18.

      Kinza Kishawishi kwa Bidii

      15. Ni nini kinachohusika katika kukinza kishawishi?

      15 Mbali na kuepuka kishawishi inapowezekana, ni lazima tukikinze kwa bidii hadi kipite au hali ibadilike. Yesu aliposhawishiwa na Shetani, alimkinza hadi Ibilisi akaenda zake. (Mathayo 4:1-11) Mwanafunzi Yakobo aliandika: “Mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia.” (Yakobo 4:7) Ukinzani unaanza kwa kuimarisha akili yetu kwa Neno la Mungu na kuazimia kwa dhati kwamba tutashikamana na viwango vyake. Tunafanya vema kukariri na kutafakari maandiko muhimu yanayozungumzia udhaifu wetu hususa. Lingekuwa jambo la hekima kutafuta Mkristo mkomavu—labda mzee—ambaye tunaweza kumwambia mahangaiko yetu na ambaye tunaweza kumwomba msaada tunaposhawishiwa kufanya jambo baya.—Mithali 22:17.

      16. Tunawezaje kudumu tukiwa wanyofu kiadili?

      16 Maandiko yanatusihi tuvae utu mpya. (Waefeso 4:24) Hilo lamaanisha kuruhusu Yehova atufinyange na kutubadili. Alipomwandikia Timotheo mfanyakazi mwenzake, Paulo alisema: “Fuatia uadilifu, ujitoaji-kimungu, imani, upendo, uvumilivu, tabia-pole. Pigana pigano bora la imani, pata mshiko imara juu ya uhai udumuo milele ambao uliitiwa.” (1 Timotheo 6:11, 12) Tunaweza “kufuatia uadilifu” kwa kusoma Neno la Mungu kwa bidii ili kupata ujuzi kamili wa utu wake, kisha kutenda kupatana na matakwa yake. Ratiba kamili ya utendaji wa Kikristo, kama vile kuhubiri habari njema na kuhudhuria mikutano, ni muhimu pia. Kumkaribia Mungu na kujinufaisha kikamili na maandalizi yake ya kiroho kutatusaidia kukua kiroho na kudumu tukiwa wanyofu kiadili.—Yakobo 4:8.

      17. Tunajuaje kwamba Mungu hatatuachilia mbali wakati wa kishawishi?

      17 Paulo anatuhakikishia kwamba kishawishi chochote kitupatacho hakitashinda uwezo tuliopewa na Mungu wa kushughulika nacho. Yehova ‘atafanya njia ya kutokea kusudi tuweze kukivumilia.’ (1 Wakorintho 10:13) Naam, Mungu haruhusu kishawishi kiwe chenye kulemea sana hivi kwamba tunakosa nguvu za kiroho za kutosha ili kudumisha uaminifu-maadili wetu ikiwa tunaendelea kumtegemea. Anataka tufaulu kukinza kwa bidii kishawishi cha kufanya yaliyo mabaya machoni pake. Isitoshe, tunaweza kuwa na imani katika ahadi hii yake: “Hakika sitakuacha kwa vyovyote wala kukuachilia mbali kwa vyovyote.”—Waebrania 13:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki