-
Tazama Zaidi ya Vitu Uvionavyo!Mnara wa Mlinzi—1996 | Februari 15
-
-
Ona Dhiki za Sasa Kuwa za Muda Tu!
Tupende tusipende, kila siku sisi huona vitu ambavyo hatungependa kuona. Tukitazama kioo ni lazima tuone kasoro na mawaa kwenye mwili wetu wa halisi, jambo lionyeshalo kutokamilika kwetu kimwili. Tuchunguliapo kioo cha Neno la Mungu, sisi huona kasoro na mawaa ya kiroho, kwetu wenyewe na vilevile kwa wengine. (Yakobo 1:22-25) Na tutazamapo gazeti la kila siku au televisheni, visa vya ukosefu wa haki, ukatili, na msiba hutokeza na kutuletea huzuni.
Shetani angependa kutukatisha tamaa kwa sababu ya vitu tuonavyo au tukengeushwe na kuanza kusita-sita katika imani. Tunaweza kuzuiaje jambo hili lisitendeke? Ni lazima tufuate kielelezo kilichowekwa na Yesu Kristo, kama mtume Petro alivyopendekeza aliposema hivi: “Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akaawachia kielelezo, mfuate nyayo zake.” (1 Petro 2:21) Katika kila hali ya maisha ya Kikristo, Yesu alikuwa kielelezo kikamilifu.
Akirejezea Yesu kuwa kiolezo chetu, Petro hasa alitaja kwamba Yesu aliteseka. Kwa kweli Yesu aliteseka sana alipokuwa duniani. Akiwa “stadi wa kazi” wa Yehova aliyekuwapo wakati wa uumbaji wa mwanadamu, yeye alijua hasa kusudi la Mungu kwa wanadamu. (Mithali 8:30, 31) Lakini sasa alijionea mwenyewe kile ambacho dhambi na kutokamilika kilichowafanya wawe. Kila siku aliona naye alilazimika kushughulikia kutokamilika na udhaifu mbalimbali wa watu. Ni lazima jambo hilo lilimletea majaribu sana.—Mathayo 9:36; Marko 6:34.
Mbali na dhiki za wengine, Yesu pia alipata dhiki. (Waebrania 5:7, 8) Lakini akiwa na macho makamilifu ya kiroho, yeye alitazama zaidi ya vitu hivyo na kuona thawabu ya kutukuzwa kwa uhai usioweza kufa kwa sababu ya mwendo wake wa uaminifu wa maadili. Kisha akiwa Mfalme wa Kimesiya, yeye angekuwa na pendeleo la kuinua wanadamu wenye matatizo kutoka kwa hali yao mbaya kurudia ukamilifu ambao Yehova alikusudia awali. Kukazia macho matazamio haya ya wakati ujao yasiyoonekana kulimsaidia kudumisha shangwe katika utumishi wa kimungu japo dhiki alizopata kila mara. Paulo aliandika baadaye: “Kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake alivumilia mti wa mateso, akidharau aibu, na ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.”—Waebrania 12:2, NW.
Yesu hakukubali kamwe hali zenye magumu na majaribu zimfanye akate tamaa, akengeushwe, au kusitasita katika imani. Tukiwa wanafunzi wake, ni lazima tufuate kielelezo chake kizuri sana.—Mathayo 16:24.
-
-
Tazama Zaidi ya Vitu Uvionavyo!Mnara wa Mlinzi—1996 | Februari 15
-
-
Paulo aliendelea kusema: “Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana;
-