-
Kushiriki Faraja Ambayo Yehova HuandaaMnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 1
-
-
“Tumaini letu kwa ajili yenu ni imara, tukijua ya kuwa kama vile mlivyo washiriki wa yale mateso, vivyo hivyo mmekuwa washiriki wa zile faraja.”—2 WAKORINTHO 1:7.
-
-
Kushiriki Faraja Ambayo Yehova HuandaaMnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 1
-
-
Hata dhiki iwe ipi, wote ambao hufuatia kwa uaminifu maisha yaliyo wakfu kwa Mungu waweza kuwa na uhakika wa jambo moja. Kwa njia ya kibinafsi sana, watapata faraja na msaada wa Mungu.
-
-
Kushiriki Faraja Ambayo Yehova HuandaaMnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 1
-
-
11 Barua ya Paulo ya pili lazima iwe ililifariji kutaniko la Korintho. Na hilo lilikuwa mojawapo makusudio yake. Yeye alieleza hivi: “Tumaini letu kwa ajili yenu ni imara, tukijua ya kuwa kama vile mlivyo washiriki wa yale mateso, vivyo hivyo mmekuwa washiriki wa zile faraja.” (2 Wakorintho 1:7) Kwenye umalizio wa barua yake, Paulo alisihi sana hivi: “Endeleeni . . . kufarijiwa, . . . na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.”—2 Wakorintho 13:11, NW.
12. Wakristo wote wana uhitaji upi?
12 Ni somo la maana kama nini tuwezalo kujifunza kutokana na hilo! Washiriki wote wa kutaniko la Kikristo wanahitaji ‘kushiriki faraja’ ambazo Mungu huandaa kupitia Neno lake, roho yake takatifu, na tengenezo lake la kidunia. Hata waliotengwa na ushirika huenda wakahitaji kupata faraja ikiwa wametubu na kurekebisha mwendo wao wenye kosa. Hivyo, “mtumwa mwaminifu mwenye akili” ameanzisha uandalizi wenye rehema wa kuwasaidia. Mara moja kila mwaka wazee wawili waweza kutembelea watu fulani-fulani waliotengwa na ushirika. Huenda hao wasionyeshe tena mwelekeo wa uasi au kuhusika katika dhambi nzito na huenda wakahitaji msaada ili kuchukua hatua za lazima za kurejeshwa.—Mathayo 24:45; Ezekieli 34:16.
-