-
“Sasa Ndio Wakati Unaokubalika Hasa”Mnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 15
-
-
6, 7. Ni heshima gani kubwa ambayo Wakristo watiwa-mafuta wamepewa leo, na ni nani wanaofanya kazi pamoja na watiwa-mafuta hao?
6 Mwanzoni mwa barua yake, Paulo alisema kuhusu heshima kubwa ambayo yeye pamoja na Wakristo wenzake watiwa-mafuta walipewa. (Soma 2 Wakorintho 5:18-20.) Alieleza kwamba waliitwa na Mungu kwa ajili ya kusudi hususa, ili kutimiza “huduma ya upatanisho,” kuwaomba watu ‘wapatanishwe pamoja na Mungu.’ Hilo lilimaanisha kuwa tena na urafiki mzuri au kujipatanisha tena na Mungu.
7 Tangu uasi katika bustani ya Edeni, wanadamu wote wametengwa mbali na Yehova. (Rom. 3:10, 23) Hali hiyo ya kutengwa mbali na Mungu imewatumbukiza wanadamu wote kwa ujumla katika giza la kiroho, na hivyo kusababisha mateso na kifo. Paulo aliandika hivi: “Tunajua kwamba uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja mpaka sasa.” (Rom. 8:22)
-
-
“Sasa Ndio Wakati Unaokubalika Hasa”Mnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 15
-
-
8. Nini kinachofanya mwito wa kujipatanisha na Mungu uwe wa pekee?
8 Kile kinachofanya mwito wa kujipatanisha na Mungu uwe wa pekee zaidi ni kwamba hata ingawa upande mmoja tu ndio uliovunja uhusiano huo—kwa sababu ya uasi wa mwanadamu katika Edeni—Mungu mwenyewe alichukua hatua ya kurekebisha uhusiano huo. (1 Yoh. 4:10, 19) Alifanya nini? Paulo alijibu hivi: “Mungu kupitia Kristo alikuwa akiupatanisha ulimwengu kwake mwenyewe, bila kuwahesabia makosa yao, naye alitukabidhi sisi lile neno la upatanisho.”—2 Kor. 5:19; Isa. 55:6.
9. Paulo alifanya nini ili kuonyesha kwamba alithamini rehema ya Mungu?
9 Kwa kuandaa fidia au dhabihu ya ukombozi, Yehova alifungua njia ili wale wanaoamini waweze kusamehewa makosa yao na kuwa tena na urafiki pamoja naye au kujipatanisha tena naye. Zaidi ya hayo, alituma wajumbe wake kuwahimiza watu kila mahali wafanye amani pamoja naye maadamu wangeweza kufanya hivyo. (Soma 1 Timotheo 2:3-6.)
-