-
Jinsi ya Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
“Kwa hiyo sisi ni mabalozi walio badala ya Kristo,” akaandika mtume Paulo. “Kama walio badala ya Kristo tunaomba: ‘Mpatanishwe pamoja na Mungu.’”a—2 Wakorintho 5:20.
4. Ni kwa njia gani Wakristo wote wa kweli wameonyesha kwamba wao ni washikamanifu kwa Ufalme wa Mungu? (Ona “Wakristo wa Mapema Hawakujihusisha.”)
4 Kwa kuwa mabalozi huwakilisha serikali au nchi fulani, hawaingilii mambo ya ndani ya nchi walikotumwa wala kujihusisha na siasa zake. Badala yake, mabalozi hutetea serikali ya nchi ambayo wanawakilisha. Ndivyo pia wanavyofanya wafuasi wa Kristo waliotiwa mafuta, ambao ‘uraia wao uko mbinguni.’ (Wafilipi 3:20) Kwa hakika, kwa sababu wamehubiri kuhusu Ufalme kwa bidii, wamewasaidia mamilioni ya “kondoo wengine” wa Kristo ‘wapatanishwe pamoja na Mungu.’ (Yohana 10:16; Mathayo 25:31-40) Kondoo wengine ni kama wajumbe wa Kristo, nao wanawaunga mkono ndugu za Yesu waliotiwa mafuta. Wakiwa kundi lenye umoja linalotetea Ufalme wa Kimasihi, vikundi vyote viwili havijihusishi hata kidogo na siasa za ulimwengu.—Isaya 2:2-4.
-
-
Jinsi ya Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
a Tangu Pentekoste 33 W.K., Kristo amekuwa Mfalme juu ya kutaniko lake la wafuasi watiwa-mafuta walio duniani. (Wakolosai 1:13) Mwaka wa 1914, Kristo aliwekwa kuwa Mfalme wa “ufalme wa ulimwengu.” Hivyo, leo pia, Wakristo watiwa-mafuta ni mabalozi wa Ufalme wa Kimasihi.—Ufunuo 11:15.
-