-
Matatizo ya Wanadamu Yatakwisha Hivi Karibuni!Mnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
Ni jambo la kushangaza kama nini! Alipotilia shaka mara ya kwanza haki ya Mungu ya kutawala, Shetani alidokeza kwamba wanadamu walioumbwa na Mungu walikuwa na kasoro—kwamba wakipatwa na mnyanyaso au kushawishiwa, wote wataasi utawala wa Mungu. (Ayubu 1:7-12; 2:2-5) Ili kudhihirisha kwa njia yenye kutokeza “fadhili yake isiyostahiliwa yenye utukufu,” mwishowe Yehova Mungu alionyesha kwamba ana imani katika wanadamu kwa kuchukua baadhi ya watoto wa familia ya Adamu yenye dhambi na kuwafanya kuwa watoto wake wa kiroho. Washiriki wa kikundi hiki kidogo wataenda kutumikia mbinguni.
-