Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matatizo ya Wanadamu Yatakwisha Hivi Karibuni!
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
    • “Kukusanya Tena Pamoja Vitu Vyote Katika Kristo”

      Mtume asema kwamba kusudi la Mungu ni “uhudumiaji [au kusimamia mambo] kwenye kikomo kamili cha nyakati zilizowekwa rasmi.” Hilo linamaanisha nini? Linamaanisha kwamba Mungu ameweka wakati ambapo atachukua hatua na hivyo ‘kukusanya tena pamoja vitu vyote katika Kristo, vitu vilivyomo katika mbingu na vitu vilivyo duniani.’ (Waefeso 1:10) Naam, Mungu ameanzisha mpango wa kupatanisha uumbaji wote mbinguni na duniani chini ya mwelekezo wake. Msomi wa Biblia J. H. Thayer asema kwamba usemi ambao umetafsiriwa ‘kukusanya tena pamoja’ unamaanisha: “Kujikusanyia tena mwenyewe . . . vitu vyote na watu wote (ambao hapo awali walitenganishwa na dhambi) ili kuwaunganisha tena katika ushirika na Kristo.”

      Jambo hilo linaonyesha kwamba Mungu anahitaji kukusanya vitu hivyo tena pamoja kwa sababu ya mtengano uliotokea hapo awali. Mapema katika historia ya mwanadamu, wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, walijiunga na Shetani Ibilisi kumwasi Mungu. Walitaka uhuru wa kujiamulia mema na mabaya. (Mwanzo 3:1-5) Kupatana na haki ya Mungu, walifukuzwa katika familia ya Mungu na kupoteza uhusiano pamoja naye. Wakasababisha hali ya kutokamilika kwa wanadamu pamoja na mambo mabaya yanayotupata leo.—Waroma 5:12.

      Uovu Waruhusiwa Uendelee kwa Muda Mfupi

      Huenda watu fulani wakauliza, ‘Kwa nini Mungu aliwaruhusu wafanye hivyo? Kwa nini hakutumia uwezo wake mkubwa na kutimiza mapenzi yake kwa nguvu, na hivyo kuzuia maumivu na mateso tunayopata leo?’ Huenda likawa jambo la kawaida kufikiri kwa njia hiyo. Lakini kutumia nguvu nyingi hivyo kungethibitisha nini? Je, ungemheshimu au ungekubaliana na mtu ambaye anapoona upinzani unaanza kutokea anaukomesha mara moja kwa sababu tu ana nguvu za kufanya hivyo? Bila shaka la.

      Kwa kweli waasi hao hawakutilia shaka uwezo wa Mungu mweza yote. Walitilia shaka hasa haki na kufaa kwa utawala wake. Ili kusuluhisha kabisa masuala hayo muhimu yaliyotokezwa, Yehova aliwaruhusu viumbe wake wajitawale kwa muda fulani bila yeye kuingilia kati. (Mhubiri 3:1; Luka 21:24) Muda huo utakapokwisha, ataingilia kati na kuitawala dunia tena. Kufikia wakati huo itakuwa dhahiri kwamba njia yake ya kutawala ndiyo njia pekee inayoweza kuleta amani, furaha, na ufanisi kwa wakazi wa dunia. Kisha waonevu wote ulimwenguni wataondolewa kabisa.—Zaburi 72:12-14; Danieli 2:44.

  • Matatizo ya Wanadamu Yatakwisha Hivi Karibuni!
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
    • Wakati ambao ameweka wa kuchukua hatua ya moja kwa moja ili kuondoa uonevu na ukosefu wa haki unakaribia. Lakini Yehova alianza kurudisha hali hizo kwenye Pentekoste 33 W.K. Jinsi gani? Wakati huo alianza kukusanya “vitu vilivyomo katika mbingu,” wale watakaotawala na Kristo mbinguni. Hao walitia ndani Wakristo huko Efeso. (Waefeso 2:4-7) Hivi karibuni zaidi, katika wakati wetu, Yehova amekuwa akikusanya “vitu vilivyo duniani.” (Waefeso 1:10) Kupitia kampeni ya kuhubiri ulimwenguni pote, anajulisha mataifa yote habari njema kuhusu Ufalme wake mikononi mwa Yesu Kristo. Wale wanaokubali wanakusanywa mahali palipo na ulinzi na uponyaji wa kiroho. (Yohana 10:16) Hivi karibuni, wakiwa katika dunia iliyosafishwa kuwa paradiso, watapata uhuru kamili kutokana na ukosefu wa haki na kuteseka.—2 Petro 3:13; Ufunuo 11:18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki