Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Maombi Yenu na Yajulishwe Mungu”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
    • 3. (a) Kama inavyoonyeshwa na sala za watumishi waaminifu wa kale, tunaweza kutaja nini katika sala? (b) Tunaweza kutoa sala za aina gani?

      3 Mtume Paulo aliwahimiza hivi Wakristo wa wakati wake: “Msihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.” (Wafilipi 4:6, 7) Biblia ina mifano mingi ya watu waliomweleza Mungu mahangaiko yao. Baadhi yao ni Hana, Eliya, Hezekia, na Danieli. (1 Samweli 2:1-10; 1 Wafalme 18:36, 37; 2 Wafalme 19:15-19; Danieli 9:3-21) Tunapaswa kuiga mfano wao. Pia, ona kwamba maneno ya Paulo yanaonyesha tunaweza kutoa sala za aina mbalimbali. Paulo alitaja kutoa shukrani, yaani, sala ya kueleza uthamini wetu kwa ajili ya mambo ambayo Mungu anatufanyia. Sala hiyo inaweza kutia ndani kutoa sifa. Dua ni sihi ya unyenyekevu inayotolewa kwa hisia nyingi. Na tunaweza pia kutoa maombi, au kuomba jambo fulani hususa. (Luka 11:2, 3) Baba yetu wa mbinguni yuko tayari kutukubali tunapomkaribia kupitia njia yoyote kati ya hizo.

  • “Maombi Yenu na Yajulishwe Mungu”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
    • Tunaweza Kuomba Nini?

      9. Tunapaswa kuhangaikia nini hasa tunaposali?

      9 Kumbuka kwamba Paulo alisema hivi: “Katika kila jambo . . . maombi yenu na yajulishwe Mungu.” (Wafilipi 4:6) Hivyo, sala za kibinafsi zinaweza kuhusisha karibu sehemu zote za maisha. Hata hivyo, katika sala zetu tunapaswa kutanguliza mapenzi ya Yehova. Danieli aliweka mfano bora kuhusiana na jambo hilo. Wakati Waisraeli walipoadhibiwa kwa sababu ya dhambi zao, Danieli alimwomba Yehova aonyeshe rehema, akisema: “Usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya . . . jina lako!” (Danieli 9:15-19, Biblia Habari Njema) Je, sala zetu pia zinaonyesha kuwa tunahangaikia hasa kutakaswa kwa jina la Yehova na kutimizwa kwa mapenzi yake?

      10. Tunajuaje kwamba inafaa kusali kuhusu mambo ya kibinafsi?

      10 Hata hivyo, inafaa pia kuomba kuhusu mambo ya kibinafsi. Kwa mfano, kama mtunga-zaburi, tunaweza kusali ili tuelewe mambo mazito ya kiroho. Alisali hivi: “Unifanye nielewe, ili nipate kuishika sheria yako nami nipate kuishika kwa moyo wote.” (Zaburi 119:33, 34; Wakolosai 1:9, 10) Yesu “alitoa dua na pia maombi kwa Yule aliyekuwa na uwezo wa kumwokoa kutoka katika kifo.” (Waebrania 5:7) Kwa kufanya hivyo, alionyesha kwamba inafaa kuomba nguvu wakati mtu anapokabili hatari au majaribu. Alipowafundisha wanafunzi wake ile sala ya mfano, Yesu alitia ndani mambo ya kibinafsi, kama vile kusamehe makosa na kupata chakula cha kila siku.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki