-
Je, Ponografia Ni Raha Isiyodhuru?Amkeni!—2002 | Julai 8
-
-
Kufikiria mambo ya kingono isivyofaa kunaweza kuathiri ibada yetu kwa Mungu. Hiyo ndiyo sababu Paulo aliandika hivi: “Kwa hiyo, fisheni viungo vya mwili wenu . . . kwa habari ya uasherati, ukosefu wa usafi, hamu ya ngono, tamaa yenye kuumiza, na tamaa, ambako ni ibada ya sanamu.”—Wakolosai 3:5.
Katika andiko hilo Paulo alionyesha kwamba hamu ya ngono inahusiana na tamaa, ambayo ni kutaka sana kuvipata vitu usivyokuwa navyo.a Tamaa ni namna ya ibada ya sanamu. Kwa nini? Kwa sababu yule anayetamani huweka kitu anachotamani mbele ya mambo mengine yote, hata Mungu. Ponografia huamsha tamaa kwa ajili ya kitu ambacho mtu hana. “Unatamani maisha ya kingono ya mtu. . . . Huwezi kuwa na jambo jingine akilini ila tu kutamani kile ambacho huna. . . . Kile tunachotamani, tunakiabudu,” akasema mwandishi mmoja wa mambo ya kidini.
-
-
Je, Ponografia Ni Raha Isiyodhuru?Amkeni!—2002 | Julai 8
-
-
a Hapa Paulo hakuwa akizungumza kuhusu hamu ya kawaida ya ngono—ile tamaa ambayo mtu huwa nayo ya kutaka kufanya ngono na mwenzi wake wa ndoa.
-