-
UtatuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kol. 1:15, 16, UV: “Naye [Yesu Kristo] ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi.”
-
-
UtatuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
(3) Je, andiko la Wakolosai 1:16, 17 (UV) linamwondoa Yesu katika vitu vilivyoumbwa, linaposema “katika yeye vitu vyote viliumbwa . . . vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake”? Neno la Kigiriki linalotafsiriwa hapa “vitu vyote” ni panʹta, namna fulani ya neno pas. Katika Luka 13:2, VB na NAJ hutafsiri “wengine wote”; BHN husema “wengine.” (Ona pia Luka 21:29 katika UV na Wafilipi 2:21 katika NAJ na BHN.) Kupatana na mambo mengine yote ambayo Biblia inasema kumhusu Mwana, NW hutoa maana ileile kwa neno panʹta katika Wakolosai 1:16, 17 hivi kwamba husema, kwa sehemu, “kwa njia yake vitu vingine vyote viliumbwa . . . Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye na kwa ajili yake.” Kwa hiyo inaonyeshwa kwamba yeye ni kitu kilichoumbwa, sehemu ya vitu ambavyo Mungu aliviumba.
-