Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Ni Vibaya Kuomboleza?
    Amkeni!—2001 | Julai 8
    • “ZAIDI YA HAYO, AKINA NDUGU, HATUTAKI NYINYI MWE WASIO NA UJUZI KUHUSU WALE AMBAO WAMELALA KATIKA KIFO; ILI MSIPATE KUWA NA MAJONZI KAMA VILE WALE WENGINE WASIO NA TUMAINI.”—1 WATHESALONIKE 4:13.

      BIBLIA huonyesha kuwa kuna tumaini kwa wafu. Ufufuo uliofanywa na Yesu, pamoja na mafundisho yake, yalielekeza kwenye wakati ambapo wafu watafufuliwa. (Mathayo 22:23-33; Marko 5:35, 36, 41, 42; Luka 7:12-16) Tumaini hilo lituathirije? Maneno ya mtume Paulo yaliyonukuliwa juu yaonyesha kwamba tumaini hilo laweza kutufariji mpendwa anapokufa.

      Ikiwa umewahi kufiwa na mpendwa wako, bila shaka uliumia kihisia-moyo. Theresa, aliyefiwa na mumewe mwenye umri wa miaka 42 muda mfupi baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo, asema hivi: “Nilishtuka sana! Mwanzoni, niliogopa sana. Kisha nilihisi uchungu mwingi ulioongezeka siku baada ya siku. Nililia sana.” Je, kuhisi hivyo kunaonyesha ukosefu wa imani katika ahadi ya Yehova ya kuwafufua wafu? Je, maneno ya Paulo yanaonyesha kwamba ni vibaya kuomboleza?

      Mifano ya Biblia ya Watu Walioomboleza

      Twapata majibu ya maswali hayo kwa kuchunguza mifano ya Biblia ya watu walioomboleza. Katika visa vingi, kulikuwa na kipindi cha kuomboleza baada ya kifo cha mshiriki wa familia. (Mwanzo 27:41; 50:7-10; Zaburi 35:14) Watu waliomboleza kwa sababu ya huzuni nyingi.

  • Je, Ni Vibaya Kuomboleza?
    Amkeni!—2001 | Julai 8
    • Hata hivyo, ijapokuwa sisi Wakristo huhuzunika kwa sababu ya kifo, hatupati majonzi “kama vile wale wengine wasio na tumaini.” (1 Wathesalonike 4:13) Hatuhuzuniki kupita kiasi kwa kuwa twaelewa vema hali ya wafu. Twajua kwamba hawana maumivu wala hawataabiki, bali ni kana kwamba wamelala usingizi mzito kwa amani. (Mhubiri 9:5; Marko 5:39; Yohana 11:11-14) Tuna hakika kabisa kwamba Yesu, aliye “ufufuo na uhai,” atatimiza ahadi yake ya kuwafufua “wote wale waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho.”—Yohana 5:28, 29; 11:24, 25.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki