-
Jinsi Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho WakeMnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
-
-
3. (a) Ni jambo gani litakalotukia wakati ujao ambalo linatajwa katika 1 Wathesalonike 5:2, 3? (b) Viongozi wa kisiasa watafanya nini, na ni nani watakaojiunga nao?
3 Paulo aliandika kuhusu moja kati ya matukio hayo ya wakati ujao katika barua yake kwa Wathesalonike. (Soma 1 Wathesalonike 5:2, 3.)
-
-
Jinsi Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho WakeMnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
-
-
Hata hivyo, kabla tu ya siku ya Yehova kuanza, viongozi wa ulimwengu watakuwa wakisema “Amani na usalama!” Huenda hilo likarejelea tukio moja au mfuatano wa matukio. Huenda mataifa yakafikiri kwamba yako karibu kusuluhisha baadhi ya matatizo yao makubwa. Namna gani kuhusu viongozi wa kidini? Wao ni sehemu ya ulimwengu, kwa hiyo inawezekana kwamba watajiunga na viongozi wa kisiasa. (Ufu. 17:1, 2) Kwa kufanya hivyo, viongozi hao wa kidini watakuwa wanawaiga manabii waongo wa kale wa Yuda. Yehova alisema hivi kuhusu manabii hao: ‘Wanasema, “Kuna amani! Kuna amani!” wakati hakuna amani.’—Yer. 6:14; 23:16, 17.
4. Tofauti na watu wengi, sisi tunatambua nini?
4 Haidhuru ni nani watakaoshiriki kusema “Amani na usalama!” tukio hilo litaonyesha kwamba siku ya Yehova iko karibu kuanza. Ndiyo sababu Paulo alisema hivi: “Akina ndugu, hamko gizani, hivi kwamba siku hiyo iwafikie ninyi kama vile ambavyo ingewafikia wezi, kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru.” (1 The. 5:4, 5) Tofauti na watu wengi, sisi tunatambua maana ya Kimaandiko ya matukio ya sasa. Unabii huu kuhusu tangazo la “Amani na usalama!” utatimia jinsi gani hasa? Ni lazima tungoje ili tuone jinsi itakavyokuwa. Kwa hiyo, acheni tuazimie ‘kukaa macho na kutunza akili zetu.’—1 The. 5:6; Sef. 3:8.
“MALKIA” AMBAYE HAJUI KWAMBA ATAHARIBIWA
5. (a) “Dhiki kuu” itaanzaje? (b) Ni “malkia” yupi ambaye hajui kwamba ataharibiwa?
5 Ni tukio gani lisiloonekana litakalofuata baadaye? Paulo alisema hivi: “Wakati watakapokuwa wakisema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa ghafula utakapokuwa juu yao mara moja.” Sehemu ya kwanza ya ‘uharibifu huo wa ghafula’ ni shambulio dhidi ya “Babiloni Mkubwa,” milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo, inayojulikana pia kuwa “yule kahaba.” (Ufu. 17:5, 6, 15)
-