Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuthamini “Zawadi Zikiwa Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • Akiliandikia kutaniko huko Thesalonike, Paulo aliwashauri washiriki wake hivi: “Mwe na staha kwa wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu na kuwasimamia nyinyi katika Bwana na kuwaonya nyinyi kwa upole;

  • Kuthamini “Zawadi Zikiwa Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • (1 Wathesalonike 5:12, 13) ‘Kufanya kazi kwa bidii’—je, hilo halifafanui wazee ambao hujitolea wenyewe bila ubinafsi kwa niaba yetu? Fikiria kidogo ule mzigo mzito ambao ndugu hawa wapendwa huubeba.

      15 Wengi wao ni wanaume wenye familia wanaolazimika kufanya kazi ili kuandalia familia zao riziki. (1 Timotheo 5:8) Ikiwa mzee ana watoto, wachanga hao huhitaji kupewa wakati na uangalifu wa baba yao. Huenda akahitaji kuwasaidia na masomo yao ya shule nyumbani, na vilevile kuwapangia wakati fulani ili waweze kutumia nguvu zao za ujana katika tafrija inayofaa. (Mhubiri 3:1, 4) Jambo muhimu zaidi ni kwamba yeye hutunza mahitaji ya kiroho ya familia yake, huongoza funzo la Biblia la familia kwa ukawaida, huhubiri pamoja nao kwenye huduma ya shambani, na kuwapeleka kwenye mikutano ya Kikristo. (Kumbukumbu la Torati 6:4-7; Waefeso 6:4) Na tusisahau kuwa mbali na madaraka hayo ambayo wengi wetu tunayo, wazee wana wajibu zaidi: kutayarisha sehemu za mikutano, kufanya ziara za uchungaji, kutunza hali njema ya kiroho ya kutaniko na ikihitajika, kushughulikia kesi za hukumu. Wengine huwa na madaraka zaidi katika makusanyiko ya mzunguko, mikusanyiko ya wilaya, ujenzi wa Majumba ya Ufalme, na katika Halmashauri za Uhusiano na Hospitali. Kwa kweli, ndugu hawa ‘wanafanya kazi kwa bidii’!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki