-
“Fulizeni Kutafuta Kwanza Ufalme”Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
5. (a) Paulo alimtia moyo Timotheo aridhike na nini, na kwa nini? (b) Shetani hutumiaje “kupenda fedha” kama mtego hatari?
5 Miaka mingi baadaye, mtume Paulo alimwandikia Timotheo, ambaye alikuwa Efeso, jiji tajiri la kibiashara. Paulo alimkumbusha hivi: “Hatukuleta kitu katika ulimwengu, wala hatuwezi kupeleka kitu chochote nje. Kwa hiyo, tukiwa na riziki na cha kujifunika, tutakuwa wenye kuridhika na vitu hivi.” Kufanya kazi ili kujipatia wewe na familia yako “riziki na cha kujifunika” ni jambo linalofaa.
-