-
Vijana—fuatieni Miradi Inayomletea Mungu HeshimaMnara wa Mlinzi—2007 | Mei 1
-
-
5. Kulingana na 2 Timotheo 3:14, 15, ni mambo gani mawili yaliyomsaidia Timotheo afanye uamuzi wa kufuatia miradi ya kiroho?
5 Ni wazi kwamba Timotheo aliamua kufuatia miradi ya kiroho. Lakini kwa nini alifanya uamuzi huo? Katika barua yake ya pili kwa Timotheo, Paulo alitaja mambo mawili yaliyomsaidia Timotheo. “Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini,” akaandika, “ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza hayo na kwamba tangu utoto mchanga umeyajua maandishi matakatifu.” (2 Timotheo 3:14, 15)
-
-
Vijana—fuatieni Miradi Inayomletea Mungu HeshimaMnara wa Mlinzi—2007 | Mei 1
-
-
Jifunze “Maandishi Matakatifu”
9. Zaidi ya kuwa na mashirika mazuri, unapaswa kufanya ili ‘kujizoeza ujitoaji-kimungu ukiwa shabaha yako’?
9 Je, utafikia miradi ya kiroho kwa sababu tu ya kuwa na mashirika mazuri? Hapana. Kama Timotheo, unahitaji kuchunguza kwa makini “maandishi matakatifu.” Labda hupendi sana kujifunza, lakini kumbuka kwamba Timotheo alipaswa ‘kujizoeza ujitoaji-kimungu ukiwa ni shabaha yake.’ Mara nyingi, wakimbiaji wanajizoeza kwa bidii sana na kwa miezi mingi ili wafikie mradi wao. Vivyo hivyo, ili kufikia miradi ya kiroho tunahitaji kujidhabihu na kujitahidi kabisa. (1 Timotheo 4:7, 8, 10) Lakini huenda ukauliza, ‘Kujifunza Biblia kunaweza kunisaidia kwa njia gani kufikia miradi yangu?’ Acha tuzungumzie njia tatu.
10, 11. Kwa nini Maandiko yatakuchochea ufikie miradi ya kiroho? Toa mfano.
10 Kwanza, Maandiko yatakupa kichocheo kinachofaa. Yanafunua utu wenye kuvutia wa Baba yetu wa mbinguni, tendo lake kuu la upendo kutuelekea, na baraka za milele ambazo atawapa watumishi wake waaminifu. (Amosi 3:7; Yohana 3:16; Waroma 15:4) Kadiri ujuzi wako kumhusu Yehova unavyoongezeka, ndivyo upendo wako kumwelekea na tamaa yako ya kujiweka wakfu kwake itakavyoongezeka.
11 Vijana wengi Wakristo wanasema kwamba kujifunza Biblia kibinafsi kwa ukawaida kumewasaidia sana kuifanya kweli iwe mali yao. Kwa mfano, Adele alilelewa katika familia ya Kikristo lakini hakujiwekea miradi yoyote ya kiroho. Anasema hivi: “Wazazi wangu walinipeleka kwenye Jumba la Ufalme, lakini sikujifunza kibinafsi au kusikiliza mikutanoni.” Baada ya dada yake kubatizwa, Adele alianza kuchukua kweli kwa uzito. “Nilijiwekea mradi wa kusoma Biblia nzima. Nilikuwa nikisoma sehemu ndogo na kisha kuandika maelezo fulani kuhusiana na sehemu niliyosoma. Bado nina maandishi yangu yote. Niliisoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.” Hilo lilimchochea Adele aweke maisha yake wakfu kwa Yehova. Ingawa amelemaa vibaya sana, kwa sasa yeye ni painia, au mweneza-injili wa wakati wote.
12, 13. (a) Kujifunza Biblia kutamsaidia kijana afanye mabadiliko gani, na jinsi gani? (b) Toa mifano ya hekima inayotumika iliyo katika Neno la Mungu.
12 Pili, Biblia itakusaidia ufanye mabadiliko yanayohitajiwa katika utu wako. Paulo alimwambia Timotheo kwamba “maandishi matakatifu” ni ‘yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’ (2 Timotheo 3:16, 17) Kwa kutafakari kwa ukawaida mambo yanayohusiana na Neno la Mungu na kutumia kanuni za Biblia, utaruhusu roho ya Mungu iboreshe utu wako. Itakuza ndani yako sifa muhimu, kama vile unyenyekevu, uvumilivu, bidii, na upendo wa kweli kwa Wakristo wenzako. (1 Timotheo 4:15) Timotheo alikuwa na sifa hizo, nazo zilimfanya awe msaada mkubwa kwa Paulo na kwa makutaniko aliyotumikia.—Wafilipi 2:20-22.
13 Tatu, Neno la Mungu ni hazina ya hekima inayotumika. (Zaburi 1:1-3; 19:7; 2 Timotheo 2:7; 3:15) Litakusaidia uchague marafiki kwa hekima, uchague burudani zinazofaa, na kukabiliana na matatizo mengine mengi. (Mwanzo 34:1, 2; Zaburi 119:37; 1 Wakorintho 7:36) Kufanya maamuzi yenye hekima sasa kutakusaidia kufikia miradi yako ya kiroho.
-