-
Sema Lililo “Jema kwa Ajili ya Kujenga”“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
7, 8. Tunawajibika kadiri gani mbele za Yehova kwa sababu ya maneno yetu?
7 Sababu ya tatu ya kuwa waangalifu kuhusu yale tunayosema ni kwamba Yehova atatuhukumu kulingana na maneno yetu. Mbali na uhusiano wetu na wanadamu wenzetu, msimamo wetu mbele za Yehova pia unategemea jinsi tunavyoutumia ulimi wetu. Andiko la Yakobo 1:26 linasema: “Ikiwa mtu yeyote anajiona kuwa mwabudu anayeshikilia vizuri namna ya ibada na bado hauongozi ulimi wake, bali anaendelea kuudanganya moyo wake mwenyewe, namna ya ibada ya mtu huyo ni ya ubatili.”b Kama tulivyoona katika sura inayotangulia, usemi wetu unahusiana sana na ibada yetu. Ikiwa hatuzuii ulimi wetu—tukiropoka maneno yenye kuumiza na yenye sumu—mambo yote tunayofanya ili kumpendeza Mungu, yanaweza kuwa bure machoni pake. Hilo ni jambo zito, sivyo?—Yakobo 3:8-10.
-
-
Sema Lililo “Jema kwa Ajili ya Kujenga”“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
b Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “ubatili” linaweza pia kutafsiriwa “bure” na “-siozaa matunda.”—1 Wakorintho 15:17; 1 Petro 1:18.
-