Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kudumisha Msimamo Wetu Tukiwa “Wakaaji wa Muda”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
    • 17 Wakristo wanafuata shauri la Petro la ‘kumheshimu mfalme’ kwa kuwatii maofisa wa umma na kuwaonyesha heshima na staha wanayostahili kulingana na vyeo vyao. (1 Pet. 2:17)

  • Kudumisha Msimamo Wetu Tukiwa “Wakaaji wa Muda”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
    • KUONYESHA UPENDO

      18. (a) Kwa nini tunafurahia kuupenda ushirika mzima wa akina ndugu? (b) Watu fulani ambao si Mashahidi wamesema nini kuwahusu?

      18 Mtume Petro aliandika hivi: “Upendeni ushirika mzima wa akina ndugu, mwogopeni Mungu.” (1 Pet. 2:17) Mashahidi wa Yehova wana woga unaofaa wa kutompendeza Mungu, nao unawachochea zaidi kufanya mapenzi yake. Wanafurahia kumtumikia Yehova wakiwa sehemu ya ushirika wa ulimwenguni pote wa akina ndugu na dada wanaotamani kufanya vivyo hivyo. Kwa hiyo, wanafurahia ‘kuupenda ushirika mzima wa akina ndugu.’ Upendo huo wa kindugu, usiopatikana kwa urahisi katika ulimwengu wa leo wenye uchoyo, unawashangaza watu ambao si Mashahidi. Kwa mfano, mfanyakazi mmoja wa shirika la Marekani la kupanga safari za watalii alishangaa kuona jinsi Mashahidi walivyowasaidia na kuwaonyesha upendo wajumbe wa nchi nyingine waliohudhuria kusanyiko la kimataifa nchini Ujerumani mwaka wa 2009. Mwanamke huyo alisema kwamba katika miaka yote ambayo amekuwa akiwatembeza watalii, hajawahi kamwe kuona jambo kama hilo. Baadaye, Shahidi mmoja alisema hivi: “Kila jambo alilosema kutuhusu alilisema kwa mshangao na msisimko.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki