-
Je, Unamwiga Yehova Katika Kuwajali Wengine?Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 15
-
-
wala si kama kwa kupiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu, bali kuwa vielelezo kwa kundi.”—1 Petro 5:2, 3.
-
-
Je, Unamwiga Yehova Katika Kuwajali Wengine?Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 15
-
-
Hata hivyo, maneno hayo ya Petro yanafunua hatari fulani, yaani, hatari ya wazee “kupiga ubwana juu ya” kutaniko. Jambo moja linaloonyesha kwamba mzee anapiga ubwana juu ya kutaniko ni kutunga sheria zisizo za lazima. Akihisi kwamba ana wajibu mkubwa wa kulinda kundi, mzee anaweza kupita mipaka. Katika kutaniko moja huko Mashariki, wazee waliweka sheria kuhusu jinsi ya kuwasalimu wengine katika Jumba la Ufalme—kama vile ni nani anayepaswa kuwa wa kwanza kutoa salamu—wakiamini kwamba kufuata sheria hizo kungeleta amani kutanikoni. Hapana shaka kwamba walikuwa na nia njema, hata hivyo, je, wazee hao walikuwa wakiiga mfano wa Yehova wa kuwajali watu wake? Ni muhimu kwamba mtazamo wa akilini wa mtume Paulo ulionyeshwa na maneno yake yafuatayo: “Si kwamba sisi ndio mabwana juu ya imani yenu, bali sisi ni wafanyakazi wenzi kwa shangwe yenu, kwa maana ni kwa imani yenu kwamba ninyi mnasimama.” (2 Wakorintho 1:24) Yehova anawatumaini watu wake.
-