-
Je, Utatii Maonyo Yaliyo Wazi Kutoka Kwa Yehova?Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
Usiwafuate “Walimu wa Uwongo”
3, 4. (a) Kwa nini walimu wa uwongo ni kama visima ambavyo vimekauka? (b) Walimu wengi wa uwongo wanatoka wapi, na wanataka nini?
3 Wazia kwamba unasafiri katika jangwa. Kwa mbali, unaona kisima, na unaenda kwenye kisima hicho kwa sababu unafikiri kwamba utapata maji ya kumaliza kiu chako. Lakini unapofika kwenye kisima hicho, unaona kwamba kimekauka. Unavunjika moyo kama nini! Walimu wa uwongo ni kama visima ambavyo vimekauka. Mtu yeyote ambaye anaenda kutafuta maji ya kweli kutoka kwao atavunjika moyo kabisa. Kupitia mtume Paulo na Petro, Yehova anatuonya kuhusu walimu wa uwongo. (Soma Matendo 20:29, 30; 2 Petro 2:1-3.) Walimu hao wa uwongo ni nani? Maneno ya mitume hao wawili yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanatusaidia kutambua walimu wa uwongo wanatoka wapi na jinsi wanavyowadanganya watu.
4 Paulo aliwaambia hivi wazee wa kutaniko la Efeso: “Kutoka katikati yenu ninyi wenyewe watu watasimama na kusema mambo yaliyopotoka.” Naye Petro alisema hivi katika barua ambayo aliwaandikia Wakristo wenzake: ‘Kutakuwa na walimu wa uwongo katikati yenu.’ Kwa hiyo, walimu wa uwongo wanatoka wapi? Wanaweza kutoka ndani ya kutaniko. Walimu hao wa uwongo ni waasi-imani.a
-
-
Je, Utatii Maonyo Yaliyo Wazi Kutoka Kwa Yehova?Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
5. Walimu wa uwongo wanatumia njia gani mbalimbali?
5 Walimu wa uwongo wanawadanganya watu jinsi gani? Njia wanazotumia zinaonyesha kwamba ni wajanja sana. Waasi-imani ‘wanaingiza kimya-kimya’ mawazo yenye kupotosha ndani ya kutaniko. Kama watu wanaofanya biashara ya magendo, wanaingiza kisiri-siri maoni ya uasi-imani kwa njia ya ujanja.
-