Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jihadharini na Walimu Wasio wa Kweli!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 1
    • 3. Ni jambo gani lililotukia wakati uliopita ambalo Petro asema litatukia tena?

      3 Baada ya Petro kuwahimiza ndugu zake wakazie uangalifu unabii, yeye asema hivi: “Hata hivyo, kulikuja pia kuwa na manabii wasio wa kweli [katika Israeli la kale], kama pia kutakavyokuwa na walimu wasio wa kweli miongoni mwenu.” (2 Petro 1:14–2:1) Watu wa Mungu wa nyakati za kale walipokea unabii wa kweli, lakini pia walilazimika kushindana na mafundisho yenye kufisidi ya manabii wasio wa kweli. (Yeremia 6:13, 14; 28:1-3, 15) “Katika manabii wa Yerusalemu,” akaandika Yeremia, “nimeona neno linalochukiza sana; hufanya zinaa; huenenda katika maneno ya uongo.”—Yeremia 23:14.

      4. Kwa nini walimu wasio wa kweli wanastahili uangamizo?

      4 Akifafanua yale ambayo walimu wasio wa kweli wangefanya katika kutaniko la Kikristo, Petro asema hivi: “Hawahawa wataleta ndani kimya-kimya mafarakano yenye kuangamiza na watakana hata mmiliki [Yesu Kristo] aliyewanunua, wakijiletea wenyewe uangamizo wa kasi.” (2 Petro 2:1; Yuda 4) Tokeo la mwisho la ufarakano huo wa karne ya kwanza ni Jumuiya ya Wakristo kama tunavyoijua leo.

  • Jihadharini na Walimu Wasio wa Kweli!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 1
    • Kuanzisha Mafundisho Yasiyo ya Kweli

      6. Ni nini huwachochea walimu wasio wa kweli, nao hujaribuje kupata wanachotaka?

      6 Kwa hekima, twaona jinsi ambavyo walimu wasio wa kweli huanzisha kufikiri kwao kulikofisidiwa. Kwanza Petro asema kwamba wanafanya hilo kimya-kimya, au katika njia ya kujificha, ya hila.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki