-
Iweke Karibu Akilini Siku ya YehovaMwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
-
-
5. Kulingana na maelezo ya Petro, ni mabadiliko gani yatakayotukia katika siku ya Yehova?
5 Petro pia anatushauri tuweke karibu akilini “kuwapo kwa siku ya Yehova, ambayo kupitia kwayo mbingu zikiwa zimewaka moto zitafumuliwa na elementi zikiwa moto sana zitayeyuka.” Serikali zote za wanadamu—“mbingu”—zitaharibiwa, ndivyo na wanadamu wote waovu—“dunia”—pamoja na “elementi” zake, yaani, mawazo na matendo ya ulimwengu huu mwovu, kama vile mwelekeo wake wa kutomtegemea Mungu na ukosefu wake wa adili na kupenda mno vitu vya kimwili.
-