-
‘Fanyeni Pigano Kali kwa Ajili ya Imani’!Mnara wa Mlinzi—1998 | Juni 1
-
-
14, 15. (a) Kujijenga wenyewe katika “imani ye[t]u takatifu zaidi” sana kwamaanisha nini? (b) Twawezaje kuchunguza hali ya silaha zetu za kiroho?
14 Kwanza, Yuda atuambia tuendelee kujijenga wenyewe katika ‘imani yetu takatifu zaidi sana.’ (Yuda 20) Kama tulivyoona katika makala iliyotangulia, hii ni hatua ya kuendelea. Sisi tuko kama majengo ambayo yanahitaji kuimarishwa dhidi ya shambulio lenye kuharibu la hali za hewa zisababishwazo na vitu vya asili. (Linganisha Mathayo 7:24, 25.) Kwa hiyo na tusiwe wenye uhakika kupita kiasi. Badala yake, acheni tuone tuwezako kujijenga kwenye msingi wa imani yetu, tukiwa askari-jeshi wa Kristo wenye nguvu zaidi, walio waaminifu. Kwa mfano, twaweza kuchunguza sehemu za suti ya kiroho ya silaha inayofafanuliwa kwenye Waefeso 6:11-18.
15 Hali ya silaha zetu wenyewe za kiroho ikoje? Je, “ngao [yetu] kubwa ya imani” ni yenye nguvu kama ipasavyo kuwa? Tutazamapo nyuma miaka ya juzijuzi, je, twaona ishara fulani za kulegea, kama vile kupunguza kuhudhuria mikutano, kukosa bidii katika huduma, au kufifia kwa shauku kwa ajili ya funzo la kibinafsi? Ishara kama hizo ni zenye hatari! Twahitaji kutenda sasa ili kujijenga na kujiimarisha katika kweli.—1 Timotheo 4:15; 2 Timotheo 4:2; Waebrania 10:24, 25.
-
-
‘Fanyeni Pigano Kali kwa Ajili ya Imani’!Mnara wa Mlinzi—1998 | Juni 1
-
-
16. Kusali tukiwa na roho takatifu kwamaanisha nini, na ni jambo gani moja tupaswalo kuomba Yehova kwa ukawaida?
16 Njia ya pili ya kubaki katika upendo wa Mungu ni kuendelea kusali tukiwa na roho takatifu. (Yuda 20) Hiyo yamaanisha kusali kwa uvutano wa roho ya Yehova na kupatana na Neno lake lililopuliziwa kwa roho. Sala ni njia muhimu ya kumkaribia Yehova kibinafsi na kueleza ujitoaji wetu kwake. Tusipuuze kamwe pendeleo hilo la ajabu! Na tusalipo, twaweza kuuliza—kwa hakika, kuendelea kuomba—tupate roho takatifu. (Luka 11:13) Ndiyo kani iliyo na nguvu zaidi tuwezayo kupata. Tukiwa na msaada huo, sikuzote twaweza kubaki katika upendo wa Mungu na kuvumilia tukiwa askari-jeshi wa Kristo.
-