-
Kushangilia Katika Tumaini LetuMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
Ingawa alikuwa na mambo mengine muhimu ya kuwaeleza, kwenye umalizio wa barua yake fupi, alirejelea tumaini zuri ajabu ambalo Wakristo watiwa-mafuta wanashiriki, aliandika hivi: “Sasa kwake yeye ambaye anaweza kuwalinda ninyi ili msijikwae na kuwaweka muwe bila dosari mbele ya utukufu wake kwa shangwe kuu, kwake Mungu pekee aliye Mwokozi wetu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu, na kuwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa umilele wote uliopita na sasa na mpaka umilele wote.”—Yuda 24, 25.
-
-
Kushangilia Katika Tumaini LetuMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
Ingawa alikuwa na mambo mengine muhimu ya kuwaeleza, kwenye umalizio wa barua yake fupi, alirejelea tumaini zuri ajabu ambalo Wakristo watiwa-mafuta wanashiriki, aliandika hivi: “Sasa kwake yeye ambaye anaweza kuwalinda ninyi ili msijikwae na kuwaweka muwe bila dosari mbele ya utukufu wake kwa shangwe kuu, kwake Mungu pekee aliye Mwokozi wetu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu, na kuwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa umilele wote uliopita na sasa na mpaka umilele wote.”—Yuda 24, 25.
-
-
Kushangilia Katika Tumaini LetuMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
8. Kulingana na andiko la Yuda 24, ni nini kinachoonyesha kwamba kuna shangwe mbinguni mmoja wa watiwa-mafuta anapodumisha utimilifu wake hadi mwisho?
8 Bila shaka, kila Mkristo mtiwa-mafuta mwaminifu anataka alindwe ili asijikwae na hivyo kuangamia. Tumaini lao linalotegemea Biblia ni kwamba Yesu Kristo atawafufua kutoka katika wafu, na kuwawezesha waonekane mbele za uso wa Mungu wakiwa viumbe wa roho wakamilifu na wenye shangwe nyingi. Mtiwa-mafuta anapokufa akiwa mwaminifu anakuwa na tumaini hakika la kwamba ‘atafufuliwa akiwa na mwili wa roho,’ atafufuliwa “katika kutoweza kuharibika . . . , katika utukufu.” (1 Kor. 15:42-44) Ikiwa kuna “shangwe zaidi mbinguni juu ya mtenda-dhambi mmoja anayetubu,” hebu wazia shangwe inayokuwa mbinguni wakati mmoja wa ndugu aliyezaliwa kwa roho wa Kristo anapomaliza mwendo wake akiwa mtimilifu. (Luka 15:7) Yehova na viumbe waaminifu wa roho watashangilia pamoja na mtiwa-mafuta ambaye atapokea thawabu yake “kwa shangwe kuu.”—Soma 1 Yohana 3:2.
-