Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kupambana na Hayawani Wawili Wakali Sana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Na yeye alipewa ruhusa kuupa pumzi huo mfano wa hayawani-mwitu, ili kwamba mfano wa hayawani-mwitu upaswe kunena na kusababisha pia kuuawa kwa wale wote ambao kwa njia yoyote hawangeabudu mfano wa hayawani-mwitu.”—Ufunuo 13:14, 15, NW.

  • Kupambana na Hayawani Wawili Wakali Sana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Hayawani-mwitu huvuvia uhai ndani ya mfano huu hivi kwamba mfano unaweza kuishi na kutimiza daraka katika historia ya ulimwengu.

      30, 31. (a) Mambo ya hakika ya historia ya ulimwengu yanautambulisha mfano huu kuwa nini? (b) Je! wowote wameuawa kwa kukataa kuabudu mfano huu? Fafanua.

      30 Kutimia kwa historia hutambulisha mfano huu kuwa tengenezo lililopendekezwa, lililoendelezwa, na kutegemezwa na Uingereza na United States na hapo kwanza likijulikana kuwa Ushirika wa Mataifa. Baadaye, katika Ufunuo sura ya 17, utatokea chini ya umbo tofauti, lile la hayawani-mwitu anayeishi, anayepumua mwenye rangi-nyekundu-nyangavu mwenye kuwako kwa kujitegemea. Hili baraza la kimataifa ‘hunena,’ katika maana ya kwamba hufanya madai ya kujisifu kuwa ndilo pekee linaloweza kuleta amani na usalama kwa aina ya binadamu. Lakini kwa uhakika kwa mataifa washiriki limekuwa baraza la kubadilishana mashutumu na matukano ya mdomo. Limetoa tisho la kutengwa mbali, au la kifo hai, kwa taifa lolote au kikundi cha watu kisichoinamia mamlaka yalo. Ushirika wa Mataifa ulifukuza mataifa ambayo yalishindwa kufuata mawazo yalo. Kwenye mwanzo wa ile dhiki kubwa, “pembe” za kivita za huu mfano wa hayawani-mwitu zitatimiza daraka lenye kukumba sana.—Ufunuo 7:14; 17:8, 16.

      31 Tangu Vita ya Ulimwengu 2, mfano wa hayawani-mwitu—sasa ukidhihirishwa kuwa tengenezo la Umoja wa Mataifa—umekwisha ua kwa njia halisi. Mathalani, katika 1950, jeshi la UM liliingia uwanjani katika vita kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini. Jeshi la UM, pamoja na lile la Korea Kusini, yaliua Wakorea wa Kaskazini na Wachina waliokadiriwa kuwa 1,420,000. Hali kadhalika, kutoka 1960 kufika 1964, majeshi ya Umoja wa Mataifa yalikuwa yakitenda katika Kongo (Kinshasa). Zaidi ya hilo, viongozi wa ulimwengu, kutia na mapapa Paul wa Sita na John Paul wa Pili, wameendelea kuthibitisha kwamba mfano huu ndio tumaini la mwisho na lililo bora kwa ajili ya amani. Aina ya binadamu ikishindwa kuutumikia, wao wanasisitiza, jamii ya kibinadamu itajiangamiza yenyewe. Hivyo kitamathali wao husababisha wauawe wanadamu wote ambao hukataa kufuatana na mfano na kuuabudu.—Kumbukumbu 5:8, 9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki